Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mheshimiwa Pierre Nkurunziza, leo tarehe 28.9.2017 ametembelea Maonesho ya Kwanza ya Biashara ya Tanzania yanayofanyika katika Viwanja vya Maonesho vya Tempete vilivyopo Mjini Bujumbura.
 
 Maonesho haya yaliandaliwa na TANTRADE kwa ushirikiano na Ubalozi wa Tanzania Burundi pamoja na Mamlaka ya Bandari Tanzania ( TPA ) yamefunguliwa rasmi tarehe 27.9.2017 na Dr Joseph Bitore, Makamu wa Pili wa Rais wa Burundi yanatarajia kumalizika tarehe 1.10.2017. 
 
Baada ya kutembelea Maonesho haya, Mh. Rais Nkurunziza alisifu uhusiano uliopo baina ya Burundi na Tanzania na aliahidi kuunga mkono juhudi zote za kuimarisha uchumi baina ya Nchi hizi mbili. 
 
Picha chini zinamuonesha Rais Nkurunzinza akiongozwa na Mh. Christopher Chiza, Mwenyekiti wa Bodi TanTrade, Balozi Rajabu Gamaha, Balozi wa Tanzania Burundi pamoja na Bw. Edwin Rutageruka, Kaimu Mkurugenzi Mkuu TanTrade ambao wapo Mjini Bujumbula kwa sasa kubudhuria Maonesho haya.

  Rais Nkurunzinza akipata maelezo mafupi kuhusu bidhaa mbalimbali zinazouzwa kwenye maonesho hayo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu TanTrade Bw. Edwin Rutageruka,ambao wapo Mjini Bujumbula kwa sasa kubudhuria Maonesho hayo.
 Rais Nkurunzinza akiongozwa na Mh. Christopher Chiza, Mwenyekiti wa Bodi TanTrade, Balozi Rajabu Gamaha, Balozi wa Tanzania Burundi pamoja na Bw. Edwin Rutageruka, Kaimu Mkurugenzi Mkuu TanTrade ambao wapo Mjini Bujumbula kwa sasa kuhudhuria Maonesho hayo.
 Mheshimiwa Pierre Nkurunziza, Rais wa Jamhuri ya Burundi, leo tarehe 28.9.2017 ametembelea Maonesho ya Kwanza ya Biashara ya Tanzania yanayofanyika katika Viwanja vya Maonesho vya Tempete vilivyopo Mjini Bujumbura.
 
 Rais Nkurunzinza akihojiwa na baadhi ya Wanahabari (hawapo pichani),kwenye maonesho hayo, kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi TanTrade, Christopher Chiza pamoja na  Kaimu Mkurugenzi Mkuu TanTrade Bw. Edwin Rutageruka,ambao wapo Mjini Bujumbula kwa sasa kubudhuria Maonesho hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...