Kumekuwa
na taarifa potofu katika mitandao ya kijamii kuwa wafuasi 11 wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilayani Ikungi walikamatwa kwa kosa la kuendesha
michango kwa ajili ya Mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Lissu
aliyejeruhiwa kwa risasi na watu wasiojulikana.
Ukweli
ni kwamba taarifa hizi ni potofu na zenye lengo la kuwafitinisha wana Ikungi na
jimbo la Singida Mashariki kwa ujumla. Viongozi waliokamatwa na ambao baadaye
walihojiwa na kuachiwa kwa dhamana hawakuwa wakiratibu michango yoyote bali
walikutwa wakiandika mabango yenye uchochezi dhidi ya viongozi wa Serikali na wakitaka
kuandamana bila kibali.
Wakati
Mhe Lissu anaendelea kupatiwa matibabu nje ya nchi na Serikali ikiwa inalifuatilia
jambo hili kwa karibu ili kuwachukulia hatua kali wote waliohusika, natoa rai
kwa wana Ikungi kuwa ni vyema tukaungana badala ya kuingiza siasa na mihemko
katika jambo hili kama Taifa lilivyoungana katika tatizo la Kibiti ambalo sasa
limemalizika.
Aidha,
kwa kuwa tayari viongozi wa kitaifa wa Chadema wameshatangaza utaratibu wa
kuchangia, nawashauri viongozi wa chama hicho wilaya kutumia mkondo huo. Vile
vile, kwa wadhifa wangu, nimeshamwagiza Mwenyekiti wa Halmashauri yetu ya Ikungi
ili aitishe kikao cha madiwani wote kuweka utaratibu wa pamoja wa namna gani ya
kuchangia matibabu ya mbunge wetu.
Nichukue
fursa hii kumpa pole Mhe. Lissu na wananchi wenzangu wa Ikungi na mahsusi jimbo
la Singida Mashariki kwa tukio hili baya. Serikali ya Wilaya inalaani vikali
wote waliohusika katika tukio hili ambalo linakwenda tofauti na mila na desturi
za Kitanzania.
Tunamwombea
Mhe Lissu nafuu ya haraka ili aweze kurejea kwenye majukumu yake ya kuwatumikia
wananchi.
Imetolewa na:
Ndugu
Miraji J. Mtaturu
Mkuu
wa Wilaya ya Ikungi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...