Na John Nditi, Ulanga.
KAMPUNI ya TanzGraphite imesema itawajengea nyumba zenye hadhi ya juu kaya za  kijiji cha Epanko, wilayani Ulanga , mkoani Morogoro  zinazohama kwa kupisha mradi mkubwa wa uchimbaji wa madini ya Kinywe (Graphite) na itahakikisha kuwa,  maisha ya watu wanaohama yanabaki kama ilivyokuwa awali ikiwa na  kuboreshwa zaidi.

Meneja Mahusiano wa TanzGraphite, Bernard Mihayo , alisema hayo kwenye taarifa ya Kampuni hiyo  katika  kikao cha tisa cha kikosi kazi kilichokutana  Septemba 14, mwaka huu  mjini Mahenge , wilayani humo.

Kikao hicho kilichokuwa ni cha kujadili na kupokea mrejesho wa vikao vya wananchi kuhusu mpango wa uhamishaji makazi (RAP) kupisha mradi wa madini ya kinywe wa Epanko kilihudhuriwa na  wajumbe  wa vitongoji vya  Kazimoto, Epanko A, Itatira , Mbera, Epanko B na Luli .

 Wawakilishi wengine ni kutoka   ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro, Ofisi ya madini mkoa , Ofisi ya  wilaya ya Ulanga , halmashauri na wadau wengine wa mradi huo.

Madini ya Graphite ‘Kinywe’ kwa sasa yanahitajika kwa wingi duniani kutokana na matumizi ya  kutengeneza vitu mbalimbali ikiwemo betri za simu , kompyuta mpakato ‘laptop’  na penseli .
 Kiongozi wa wa kimila wa kabila la Wapogoro wa kijiji cha Epanko , wilaya ya Ulanga, mkoani Morogoro  (Mbuyi ), Redemta Masura ( wapili kushoto) akiwa na viongozi  wa Kijiji hicho wakipitia  taarifa  ya mpango wa uhamishaji makazi kupisha mradi wa madini ya Kinywe wa Epanko , wakati wa kikao cha tisa cha Kikosi Kazi iliyowashirikiasha wajumbe wa kutoka vitongozi sita wa kijiji hicho , viongozi kiserikali na kijamii kilichofanyika hivi karibuni mjini Mahenge.
 Baadhi ya viongozi wa serikali wa wilaya ya Ulanga na mkoa wa Morogoro wakiungana na vitongoji vya kijiji cha Epanko wakiwemo na wakimila na kijamii  kupitia   taarifa  ya mpango wa uhamishaji makazi kupisha mradi wa madini ya Kinywe wa Epanko katika kikao cha tisa cha Kikosi Kazi cha mpango wa uhamishaji makazi  kupisha mradi wa madini ya Kinywe wa Epanko kilichofanyika hivi karibuni mjini Mahenge.
 Baadhi ya viongozi wa kamati ya Kikosi kazi  kutoka serikali  za vitongoji vya kijiji cha Epanko wakiwemo wa kimila na kijamii  wilayani  Ulanga  wakijumuika na wa ngazi ya wilaya hiyo na mkoa wa Morogoro kupitia   kwa pamoja taarifa  ya mpango wa uhamishaji makazi kupisha mradi wa madini ya Kinywe wa Epanko  kilichofanyika hivi karibuni mjini Mahenge.
Katibu Tawala Msaidizi Miundombinu Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Lucas Mwaisaka (kulia) akimkabidhi  Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Epanko, Kata ya Nawenge, wilayani Uanga, Eliza Liwemba, ( kushoto) Mpango wa Uhamishaji Makazi (RAP) wa Mradi wa Madini wa Epanko  wakati wa kikao cha tisa cha Kikosi Kazi cha mpango huo kilichowashirikisha wajumbe wa kutoka vitongozi sita wa kijiji hicho , viongozi kiserikali  ya wilaya  na  mkoa ambacho kilifanyika hivi  karibuni mjini Mahenge. ( Picha na John Nditi).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...