Mkuu wa Mkoa wa Singida amewataka watumishi wa umma wote mkoani hapa kulima ekari moja ya korosho ili kutunza mazingira, kujiongezea kipato pamoja na kuonyesha mfano kwa wananchi wengine ili waweze kulima zao hilo kwa ufanisi.
Dkt Rehema Nchimbi ametoa agizo hilo mapema wiki hii mara baada ya kutembelea na kukagua shamba la mkulima wa zao hilo Juma Patrick katika kijiji cha Sanjaranda halmashauri ya wilaya ya Itigi.
Dkt Nchimbi amesema kuongoza ni kuonyesha njia hivyo watumishi wa umma wanatakiwa kuonyesha njia kwa kulima vizuri hasa katika mazao ya biashara yanayopewa kipaumbele kitaifa ambapo kwa mkoa wa Singida ni korosho, pamba na tumbaku.
“Watumishi hamuwezi kuwaambia wakulima walime korosho au pamba wakati wewe haujalima wala haufahamu changamoto na faida za kilimo hicho, naagiza kila mtumishi alime ekari moja ya korosho ili muwe mabalozi wazuri wa zao hilo mkoani hapa”, amesisitiza Dkt Nchimbi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akisisitiza jambo wakati akikagua shamba la korosho la mkulima Juma Patrick wa Kijiji cha Sanjaranda halmashauri ya Wilaya ya Itigi.
Mkulima Juma Patrick wa Kijiji cha Sanjaranda halmashauri ya Wilaya ya Itigi akimuonyesha Mkuu wa Mkoa wa Singida mikorosho iliyostawi katika shamba lake.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Miraji Jumanne Mtaturu wakiwa katika shamba la korosho la mkulima Juma Patrick wa Kijiji cha Sanjaranda halmashauri ya Wilaya ya Itigi.
Shamba la mikorosho lenye ukubwa wa ekari 11 la mkulima Juma Patrick lililoko halmashauri ya Wilaya ya Itigi likiwa limestawi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...