Benny Mwaipaja, Dodoma

MAKAMU wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, anayeshughulikia masuala ya nishati Bw. Amadou Hott amesema kuwa Tanzania iko katika njia sahihi kutaka iwe na asilimia 16 ya hisa kwenye miradi inayowekezwa katika sekta ya madini na mafuta ili rasilimali hizo ziweze kuwanufaisha wananchi na wawekezaji.

Makamu huyo wa Rais ametoa kauli hiyo mjini Dodoma alipofanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango kuhusu namna benki hiyo inavyoweza kusaidia kulikwamua Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (TANESCO) kutoka katika mzigo wa madeni unaolikabili ili liweze kujiendesha kibiashara bila kutegemea ruzuku kutoka Serikalini.

Alisema kuwa nchi kadhaa duniani, zenyewe ama kwa kutumia kampuni ilizoziteua zina hisa ya kati ya asilimia 14 hadi 16 za hisa za bure katika miradi ya rasilimali za madini ili pande zote zinazohusika katika mikataba hiyo ziweze kunufaika na rasilimali za nchi.

Alitolea mfano wa baadhi ya nchi ikiwemo Senegal ambazo zinatekeleza sera kama hizo na hakuna matatizo yoyote kati ya nchi hizo na wawekezaji na kwamba anaona nia njema ya Tanzania katika kulinda rasilimali zake.

“Jambo la msingi linalotakiwa ni kuhakikisha kuwa makubaliano ya suala hili kati ya Serikali na Sekta binafsi yawe ya wazi, usawa na haki na ni muhimu wawekezaji wakakubaliana na utaratibu huo” aliongeza Bw. Hott.
Baadhi ya viongozi wa Wizara ya Fedha na Mipango wakiongozwa na Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (wa tatu kushoto) wakiwa katika mkutano na ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) ulioongozwa na Makamu wa Rais wa Benki hiyo Bw. Amadou Hott, (wa tatu kulia), Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) anayeshughulikia masuala ya nishati, Bw. Amadou Hott (kushoto) akisikiliza kwa makini wakati wa mkutano na Waziri wa fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) mkoani Dodoma, kulia ni Mkurugenzi wa benki hiyo anayeshughulika masuala ya maendeleo ya mifumo ya umeme, Bw. Henry Baldeh.
Baadhi ya viongozi wa Wizara ya Fedha na Mipango wakiongozwa na Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) wakiwa katika mkutano na ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) mjini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (kushoto) akichukua kumbukumbu wakati wa mkutano na ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) (hawapo pichani) kulia ni Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara hiyo Bw. John Rubuga, mjini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Dorothy Mwanyika (kulia), akichukua kumbukumbu wakati wa mkutano na ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) (hawapo pichani) kushoto ni Kamishna wa Bajeti wa Wizara hiyo Bi. Marry Maganga akisikiliza kwa makini wakati mkutano ukiendelea katika ukumbi wa Wizara hiyo mjini Dodoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...