Mteja wa benki ya TIB, Irene Kiwia  pamoja na wateja wengine wakishirikiana kukata keki kwaajili ya kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka Oktoba.


BENKI ya biashara  inayomilikiwa na Serikali ya Tanzania Investment Bank (TIB) inaendelea kutoa huduma mbalimbali za kibenki zenye ubunifu wa hali ya juu ili kufikia dira ya kuwa benki  ambayo ni chaguo la wateja.

Hayo yamesemwa ka Mkurugenzi mtendaji wa benki ya TIB, Frank Nyabundege wakati akizungumza na wateja wa benki ya TIB waliofika katika tawi la Samora jijini Dar es Salaam leo. Amesema kuwa benki hiyo inatoa huduma za TIB mobile, Utoaji wa bure wa dhamana za kibenki, sms alert, Premier banking, uboreshaji wa kazi za ATM, kutua huduma masaa 24 ya katika tawi la bandari, huduma za malipo ya kodo kirahisi pamoja na JIPANGE Plan.

Amesema kuwa "Huu ni mwaka ni waka wetu wa pili tangia kupata kibali cha kutoa huduma za kibenki na kuendelea kujenga uwezo wa kuwapa wateja huduma za kipekee."

Amesema kuwa hudum nzuri kwa wateja ndio kipaumbele katika maendeleo ya benki hiyo.
Mteja wa benki ya TIB, Irene Kiwia akizungumza na Michuzi TV jijini Dar es Salaam leo wakati alipofika katika benki ya TIB jijini Dar es Salaam wakati wa kuwashukuru wateja wa benki hiyo.
Mkuu wa masoko na mahusiano wa Benki ya TIB, Theresia Soka akizungumza na wateja pamoja na wafanyakazi wa benki ya TIB waliofika katika benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. 
Amewashukuru  wateja wa benki hiyo kufka katika taw la Samora kwaajili ya kusheherekea pamoja wiki ya huduma kwa wateja pamoja na kuwaomba kutoa maoni yao ili kwenye mapungufu wajirekebisha.
Baadhi ya wateja na wafanyakazi wa benki ya TIB wakiwa katika hafla fupi ya kuwashukuru wateja wao katika wiki ya huduma kwa wateja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...