Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (kushoto), akiwa ameongozana na kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa,(ACP) Julius Mjengi (kulia), alipowasili katika mkoa huo ikiwa ni muendelezo wa ziara yake za kikazi yenye lengo la kuzungumza na maofisa na askari wa Jeshi hilo na kuona changamoto zao na namna ya kuwasaidia. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akikagua gwaride maalum lililoandaliwa kwa ajili yake alipowasili mkoani Iringa, kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kuzungumza na maofisa na askari wa Jeshi hilo na kuona changamoto zao na namna ya kuwasaidia.
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiwa tayari kwa kumpokea Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, ambaye yupo mkoani Iringa, kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kuzungumza na maofisa na askari wa Jeshi hilo na kuona changamoto zao na namna ya kuwasaidia.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza, na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, wakiwa katika kikao kazi na wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama wakijadiliana namna ya kukabiliana na matukio ya uhalifu na wahalifu mkoani humo, IGP Sirro yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya siku moja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...