Na
Mathias canal, Singida
Wajumbe wa Mkutano mkuu maalumu wa Chama Cha
Mapinduzi Wilaya ya Singida Vijijini Mkoani
Singida wametumia haki yao ya kidemokrasia kwa kufanya uchaguzi wa kuwapata
viongozi wa ngazi mbalimbali za Wilaya, wawakilishi wa ngazi ya mkoa na Taifa.
Mkutano huo ulifanyika katika Kijiji na Kata ya
Ilongelo na kuhudhuruwa na wajumbe waliozidi akidi ya matakwa ya mkutano wa CCM
Wilaya kwa mujibu wa maelekezo ya kanuni za uchaguzi wa CCM.
Mwenyekiti mpya wa CCM Wilaya ya Manyoni
aliyechaguliwa kwa kura za kishindo ni William Mwang'ima Nyalandu aliyepata
kura 440, akifatiwa na FATUMA Ihonde aliyepata kura 189 na nafasi ya tatu
ilikamatwa na Alex Mdidi Lissu aliyepata kura 159.
Akizungumza na Mtandao wa www.wazo-huru.blogspot.com Katibu
wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Singida Vijijini Bi Grace Shindika alisema
kuwa uchaguzi huo umekamilika kwa amani na salama kwa kufuata taratibu na
kanuni za uchaguzi zilizoelekezwa na Chama Cha Mapinduzi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...