Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 28 Novemba, 2017 amemjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu anayepata matibabu katika hospitali ya Nairobi nchini Kenya.
Mhe. Samia Suluhu Hassan amemfikishia salamu za pole kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ambaye amemtakia matibabu mema na kupona haraka ili arejee nyumbani na kuendelea na majukumu yake.
Mhe. Tundu Lissu amemshukuru Mhe. Rais Magufuli na Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kumjulia hali na amewatakia heri katika majukumu yao.
“Msalimu Mhe. Rais mwambie namshukuru sana kwa salamu zake na kunijulia hali” amesema Mhe. Tundu Lissu.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu alipofika hospitalini hapo kumjulia hali leo tarehe 28 Novemba, 2017 jijini Nairobi nchini Kenya.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu alipofika hospitalini hapo kumjulia hali leo tarehe 28 Novemba, 2017 jijini Nairobi nchini Kenya. Kushoto ni mke wa Mhe. Lissu, Alicia Magabe na kulia ni msaidizi wa Makamu wa Rais Bw. Waziri
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo na Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu, Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dk Pindi Chana (kulia) walipofika hospitalini hapo kumjulia hali. Kushoto ni mke wa Mhe. Lissu, Bi. Alicia Magabe na wa pili kulia ni msaidizi wa Makamu wa Rais Bw. Waziri
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu alipofika hospitalini hapo kumjulia hali. Kushoto ni mke wa Mhe. Lissu, Bi. Alicia Magabe 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...