Na Hamza Temba - Wizara ya Maliasili
..........................................................................
Naibu Waziri wa
Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga amesisitiza agizo la Serikali lililotolewa
hivi karibuni na Waziri Mkuu kuhusu kukamilisha zoezi la uwekagi wa vigingi vya
mpaka kwenye maeneo ya hifadhi nchini ifikapo Desemba 31 mwaka huu.
Amesema lengo la kukamilisha
zoezi hilo ni kuiwezesha Serikali kufanya uamuzi wa mwisho wa kumaliza migogoro
ya ardhi iliyodumu kwa muda mrefu baina ya vijiji na maeneo ya hifadhi nchini.
Mhe. Hasunga ametoa
kauli hiyo jana wakati wa ziara yake ya kikazi katika hifadhi ya msitu wa
Isalalo Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe ambapo aliziagiza taasisi zilizo chini ya
Wizara yake kukamilisha zoezi hilo kabla ya tarehe hiyo ili kuiwezesha Serikali
kubaini maeneo yenye mapungufu na kuyatolea uamuzi.
“Ifikapo tarehe 31
tuwe tumemaliza kuweka hizo beacon (vigingi) za mipaka, baada ya hapo hatua
itakayofuata, Serikali tutakaa na kuangaliza ni vijiji vingapi au maeneo gani
yameingia ndani ya hifadhi, tuangalie je tuwaachie hayo maeneo wananchi au
tuwahamishe tuwapeleke maeneo mengine, maamuzi hayo yatakuja baada ya kufanya
tathmini na kubaini penye mapungufu.
“Sasa ikitokea kwamba
imefika tarehe 31 hatujatekeleza hili mimi kama Naibu Waziri nitakuwa sina
kazi, maana sijatekeleza agizo la Serikali, kwahiyo lazima tulisimamie, na mimi
sasa kabla halijanipasukia nitakupasukia bwana Meneja (Meneja TFS Wilaya ya
Mbozi), nitakuja kukagua mipaka, na kabla ya tarehe 31 nitakuja kukagua tena,”alisema
Naibu Waziri Hasunga.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akioneshwa ramani ya Hifadhi ya Msitu wa Isalalo na Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Wilaya ya Mbozi, Fred Mgeni (kulia) wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua hifadhi hiyo kwa ajili ya kuimarisha uhifadhi mkoani Songwe jana.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, John Palingo wakati wa kukagua Hifadhi ya Msitu wa Isalalo Mkoani Songwe kwenye ziara yake ya kikazi ya kuimarisha uhifadhi mkoani humo jana.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...