Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii
JUMUIYA ya Watu wa China nchini Tanzania kwa kushirikiana na Watanzania wameandaa tamasha la michezo ikiwa sehemu kudumisha umoja na ushirikiano wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili.
Tamasha hilo linahusisha michezo mbalimbali na kivutio kikubwa kilikuwa kwenye mchezo wa mpira wa Aside 5 ambao kwa hapa nchini bado haujafahamika zaidi.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa tamasha hilo lililofanyika Uwanja wa Ndani eneo la Uwanja wa Taifa ,Katibu wa Siasa wa Ubalozi wa China nchini,Yang Tong amesema kuwa nchi hizo mbili zinatambua umoja na mshikamano uliopo kwa muda mrefu na anafurahia kuona ukiimarika siku hadi siku.
Amesema kwa kutumia tamasha hilo ambalo linahusisha jumuiya ya Watu wa China na Watanzania ni fursa nyingine ya kuendelea kudumisha urafiki uliopo kwenye nchi hizo kwa muda mrefu.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Michezo wa Wizara habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo, Alex Nkeyenge akizungumza katika uzinduzi Tamasha la michezo kati ya Tanzania na China lilofanyika katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.
Mchezaji wa zamani na Kocha wa Timu ya Taifa Stars, Boniface Mkwasa akizungumza juu ya mchezo wa mpira wa miguu wa A side 5 uliochezwa katika katika tamasha la michezo kati ya Tanzania na China leo jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Siasa wa Ubalozi wa China nchini,Yang Tong akizungumza katika tamasha la michezo kati ya Jumuiya ya watu wa china na Tanzania juu uhusiano wa Tanzania na China ambao kwa sasa unakwenda hadi katika michezo, leo jijini Dar es Salaam.
Wachezaji wa karate wakionyesha umahiri wao katika tamasha la michezo kati ya Jumuiya ya Watu wa China na Tanzania leo jijini Dar es Salaam.
Kikundi cha mziki cha jumuiya ya watu wa china wakionyesha umahiri wao katika tamasha la michezo kati ya jumuiya ya watu wa china na Tanzania leo jijini Dar es Salaam.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...