Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameagiza utekelezaji wa Kampeni ya Taifa ya Usafi wa Mazingira uwe ni ajenda ya kudumu ya kila ngazi ya Uongozi.
Makamu wa Rais ameyasema hay oleo wakati wa Uzinduzi wa Kamapeni ya Taifa ya Usafi wa Mazingira awamu ya Pili ukiofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chang’ombe,mkoani Dodoma.
Makamu wa Rais alisema Serikali imejiwekea mikakati mbali mbali ya kupambana na maradhi ya kuambukiza ambapo usafi wa mazingira ni njia mojawapo ambapo katika awamu ya kwanza ya kampeni ya Taifa ya Usafi wa Mazingira ambapo jumla ya kaya 1,662,550 zilijengwa vyoo na shule 2,133 vilijengwa vyoo bora.
Katika awamu ya Pili iliyozinduliwa leo kaya 5,600,000 zinatarajiwa kuongeza idadi ya vyoo bora na shule za msingi 3,500 na sekondari 700 zitapata huduma ya vyoo bora na sehemu maalum ya kunawa mikono baada ya kutoka chooni.
“Wahenga walisema Samaki mkunje angali mbichi, methali hii inatukumbusha jukumu la kuwafundisha watoto wetu umuhimu wa usafi wa mazingira tangia wadogo wakiwa mashuleni”alisisitiza Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais alitoa Wito kwa Wanawake wote nchini kujifunga Kibwebwe na kujenga vyoo, alisema Wanawake wamekuwa na vikundi mbali mbali vya kusaidiana na kuwezeshana hivyo kwa kupitia vikundi hivyo wanaweza kufanikisha ujenzi wa vyoo bora majumbani.
Makamu wa Rais aliwapongeza Washindi wote wa Afya na Usafi wa Mazingira kwa mwaka 2016/17. Pia aliwashukuru wadau mbali mbali ambao wamechangia kwa namna moja au nyingine kufanikisha uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya Taifa ya Usafi wa Mazingira.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu mbele ya mfano wa Choo bora mara baada ya kuzindua kampeni ya Taifa ya usafi wa mazingira awamu ya pili, iliyozinduliwa rasmi kwenye viwanja vya shule ya msingi ya Chang'ombe mkoani Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akipokea mfano wa funguo kwa ajili ya kumkabidhi Mgeni rasmi Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan ikiwa ni sehemu ya ishara ya kuzinduliwa mfano wa Choo bora ndani ya uzinduzi wa kampeni ya Taifa ya usafi wa mazingira awamu ya pili, iliyozinduliwa rasmi kwenye viwanja vya shule ya msingi ya Chang'ombe mkoani Dodoma.
Makamu wa Rais ameyasema hay oleo wakati wa Uzinduzi wa Kamapeni ya Taifa ya Usafi wa Mazingira awamu ya Pili ukiofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chang’ombe,mkoani Dodoma.
Makamu wa Rais alisema Serikali imejiwekea mikakati mbali mbali ya kupambana na maradhi ya kuambukiza ambapo usafi wa mazingira ni njia mojawapo ambapo katika awamu ya kwanza ya kampeni ya Taifa ya Usafi wa Mazingira ambapo jumla ya kaya 1,662,550 zilijengwa vyoo na shule 2,133 vilijengwa vyoo bora.
Katika awamu ya Pili iliyozinduliwa leo kaya 5,600,000 zinatarajiwa kuongeza idadi ya vyoo bora na shule za msingi 3,500 na sekondari 700 zitapata huduma ya vyoo bora na sehemu maalum ya kunawa mikono baada ya kutoka chooni.
“Wahenga walisema Samaki mkunje angali mbichi, methali hii inatukumbusha jukumu la kuwafundisha watoto wetu umuhimu wa usafi wa mazingira tangia wadogo wakiwa mashuleni”alisisitiza Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais alitoa Wito kwa Wanawake wote nchini kujifunga Kibwebwe na kujenga vyoo, alisema Wanawake wamekuwa na vikundi mbali mbali vya kusaidiana na kuwezeshana hivyo kwa kupitia vikundi hivyo wanaweza kufanikisha ujenzi wa vyoo bora majumbani.
Makamu wa Rais aliwapongeza Washindi wote wa Afya na Usafi wa Mazingira kwa mwaka 2016/17. Pia aliwashukuru wadau mbali mbali ambao wamechangia kwa namna moja au nyingine kufanikisha uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya Taifa ya Usafi wa Mazingira.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu mbele ya mfano wa Choo bora mara baada ya kuzindua kampeni ya Taifa ya usafi wa mazingira awamu ya pili, iliyozinduliwa rasmi kwenye viwanja vya shule ya msingi ya Chang'ombe mkoani Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akipokea mfano wa funguo kwa ajili ya kumkabidhi Mgeni rasmi Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan ikiwa ni sehemu ya ishara ya kuzinduliwa mfano wa Choo bora ndani ya uzinduzi wa kampeni ya Taifa ya usafi wa mazingira awamu ya pili, iliyozinduliwa rasmi kwenye viwanja vya shule ya msingi ya Chang'ombe mkoani Dodoma.

Mgeni Rasmi,Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwenye moja ya banda lililokuwa likionesha baadhi ya vifaa vinavyotumika katika suala zima la usafi wa mazingira,alipopita kukagua mabanda mbalimbali yaliyokuwepo uwanjani hapo kabla ya uzinduzi wa kampeni ya Taifa ya usafi wa mazingira awamu ya pili, iliyozinduliwa rasmi kwenye viwanja vya shule ya msingi ya Chang'ombe mkoani Dodoma.

Sehemu ya Wananchi mbalimbali waliojitokeza katika uzinduzi huo mapema leo mkoani Dodoma

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Taifa ya usafi wa mazingira awamu ya pili, iliyozinduliwa rasmi kwenye viwanja vya shule ya msingi ya Chang'ombe mkoani Dodoma.

Sehemu ya zawadi mbalimbali walizokabidhiwa watu,taasisi na vikundi mbalimbali vilivyofanya vizuri katika suala zima usafi wa mazingira sambamba na vyoo bora,zawaidi hizo kama vile vyeti,piki piki pamoja na matrekta


Kikundi cha ngoma kikitumbuiza kabla ya uzinduzi wa kampeni hiyo.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...