Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamkala ya Usafiri wa Anga (TCAA), Valley Chamuluyu amesema kuwa waongoza ndege wameaswa  kutumia taaluma zao katika maendeleo ya taifa.

Chamuluyu ameyasema hayo wakati akifungua mkutano mkuu wa Chama cha Waongoza Ndege uliofanyika katika ukumbi wa mamlaka wa TCAA leo jijini Dar es Salaam, amesema TCAA itaendelea kutoa ushirikiano kwa chama cha waongoza ndege katika usimamizi wa usafiri wa anga.

Amesema kuwa waongoza ndege ni watu muhimu katika maendeleo ya taifa ambapo kazi hiyo ndiyo wanafanya usalama wa usafiri wa ndege na taifa kupata uchumi.

Nae Rais wa Chama cha Waongoza Ndege nchini (TATCA), John Msagga amesema kuwa mkutano huo watajadili mada mbalimbali ikiwemo maadili ya taaluma hiyo.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamkala ya Usafiri wa Anga (TCAA), Valley Chamuluyu akizungumza jambo wakati akifungua mkutano wa chama cha waongoza Ndege uliofanyika ukumbi wa Mamlaka ya TCAA jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Chama cha Wongoza Ndege nchini (TATCA), John Msagga akitoa taarifa za utekelezaji wa majukumu ya chama kwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Chama cha Waongoza Ndege Nchini Kenya (KATCA), Peter Oduer akizungumza juu ya ushirikiano wa chama cha waongoza Ndege Tanzania, leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Waongoza Ndege wakiwa katika mkutano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...