Ujumbe wa chama cha wamiliki wa magari ya mizigo pamoja na chama cha Mawakala wa Forodha (TAFFA) upo Dubai katika ziara ya kuitangaza bandari ya Dar es salaam kwenye falme za kiarabu (UAE).
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu chama cha Mawakala wa Forodha (TAFFA) Bw. Tony Swai nia ya ziara hiyo ni kuipromote Bandari ya Dar es Salaam pamoja na kukutana na wateja ambao wana-export na ku-import mizigo yao kuja na kutoka Kampala, Uganda.
Mwenyekiti wa wamiliki wa Magari yabebayo Mizigo kutoka Bandari ya Dar es ealaam Bi. Angelina Ngalula akiongea na Balozi Nimisha Madhavan Balozi wa Uganda katika Falme za Kiarabu (UAE) mjini Dubai jana. Kushoto ni Katibu Mkuu chama cha Mawakala wa Forodha (TAFFA) Bw. Tony Swai pamoja na Bw. Ordreck Rwabogo mwakilishi wa Mamlaka ya Bandari Uganda na Jimmy Kutosi Mwakilishi wa Uganda Board of Exporters
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...