Na Joel Maduka-Chato. 

Mkazi wa kijiji cha Minkoto Wilaya ya Chato Mkoani Geita Bw Hoja Kasumbakabo ( 25) anatuhumiwa kumuua mke wake Spensioza Petro (22) kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali mwilini na kisha kumnyonga mtoto Brison Hoja mwenye umri wa miezi mitatu kisha kutokomea kusikojulikana.

Mwenyekiti wa kijiji hicho leo Nkwabi amesema tukio hilo limetokea Januari  24,2018 kuamkia Januari 25 ,kwenye kijiji hicho ambapo ilibainika miili kuonekana chini ya Sakafu ndani ya chumba walichokuwa wanaishi huku mwili wa mwanamke huyo ukiwa na majeraha sehemu ya kooni, mgongoni na tumboni huku utumbo ukiwa nje.

Mzazi wa marehemu Mzee Petro Lusaga ameelezea kusikitisha na tukio hilo na kwamba hakuwahai kuwaona marehemu na mumewe wakiwa na ugomvi kwani kwa kipindi chote walikuwa wakiishi kwa amani bila ya kuwa na malumbano wala kelele zozote ndani ya familia yao. 
Baadhi ya wananchi wakiwa kwenye eneo ambalo kumetokea tukio. 
Jirani wa Familia ambapo kumetokea mauaji Bi,Mariam Shija akizungumza na waandishi wa habari kwa masikitiko juu ya tukio hilo. 
Diwani wa Kata Minkoto , Bw Geroge Magezi akiwasisitiza wananchi kushiriana na jeshi la Polisi kwenye suala la ulinzi na usalama. 
Dk Masanja Mchanganya anayetokea kituo cha afya cha Bwanga akielezea namna ambavyo wamebaini mwili wa marehemu majeraha yaliyopo baada ya kufanya uchunguzi.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...