Jeneza lenye mwili wa Marehemu Mama Peras Ngombale Mwiru (Mama Kinje), Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru ukiwasili kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam, alikopumzishwa kwenye nyumba yake ya milele. Mama Peras (Mama Kinje) amezikwa jioni ya leo kwenye makaburi Kinondoni, huku viongozi mbalimbali wa Kitaifa na Vyama vya siasa wakishiriki mazishi hayo.
 Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akiwa na familia ya Marehemu, wakishuhudia Jeneza lenye mwili wa Mama Peras Ngombale Mwiru likishushwa kaburini, wakati wa mazishi yake yaliyofanyika jioni ya leo kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam. Kushoto kwake ni Mtoto wa Marehemu Mama Peras, Kinje Ngombale Mwiru aliyeambatana na mkewe.
 Mume wa Marehemu Mama Peras Ngombale Mwiru, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akiweka udongo kwenye kaburi ya Mke wake mpendwa, wakati wa mazishi yake yaliyofanyika jioni ya leo kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
 Mtoto wa Marehemu Mama Peras, Kinje Ngombale Mwiru na Mkewe Anitha wakiweka udongo kwenye kaburi la Mama yao. 
 Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akiweka udongo kaburini.
Askofu akiweka msalaba kaburini.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa na Mkewe Mama Regina wakiweka shada ya maua kwenye kaburi la Mama Peras Ngombale Mwiru (Mama Kinje), Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru
 Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba na Mkewe wakiweka shada ya maua kwenye kaburi la Mama Peras Ngombale Mwiru (Mama Kinje), Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru
Mama Anna Mkapa akiweka shada ya maua kwenye kaburi la Mama Peras Ngombale Mwiru (Mama Kinje), Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...