MKUU wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, amewaonya baadhi ya watu wanaohamasishana kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii kuhusu kufanya maandamano bila kufuata utaratibu uliopo na kwamba kitendo hicho ni kinyume cha sheria za nchi.
IGP Sirro amesema hayo akiwa Bariadi Mkoani Simiyu wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi ambapo ameonya harakati zenye kuhatarisha amani ya nchi huku akitoa wito kwa wazazi kuendelea kujenga malezi bora kwa watoto wao.

Hata hivyo IGP Sirro amewataka askari wa Jeshi hilo kote nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa kufuata misingi ya sheria na taratibu za nchi ikiwa pamoja na kuhakikisha wanatenda haki kwa wananchi wanaowahudumia na kutokujihusisha na vitendo vya rushwa pamoja na kudhibiti matishio ya aina yeyote yatakayojitokeza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...