Na Hamza Temba-WMU-Manyara
........................................................................
Serikali italipa fidia na vifuta jasho kwa vitongoji ambavyo
vipo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Pori la Akiba Mkungunero ili
viweze kupisha maeneo hayo yaendelee kuhifadhiwa kwa mujibu wa sheria.
Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk.
Hamisi Kigwangalla katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kijiji cha
Kimotorok katika wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara ambao ulihudhuriwa pia na
Wakuu wa Wilaya za Simanjiro, Kiteto na Kondoa.
Alisema fidia hiyo italipwa kwa vitongoji viwili vya kijiji cha
Irkishbo vya Maasasi na Lumbenek vilivyopo katika Wilaya ya Kiteto mkoani
Manyara ambavyo vilikutwa ndani ya Pori la Akiba Mkungunero wakati pori hilo
linaanzishwa mwaka 1996 kwa Tangazo la Serikali Na. 307.
Waziri wa Maliasili
na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiongozwa na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya
Taifa ya Tarangire, Herman Batiho kukakua maeneo hifadhi hiyo jana wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutatua changamoto
za uhifadhi mkoani Manyara.
Waziri wa Maliasili
na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akionyeshwa mpaka wa Hifadhi ya Taifa ya Tarangire
na viongozi wa hifadhi hiyo wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutatua
changamoto za uhifadhi mkoani Manyara jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiongozwa na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Tarangire, Herman Batiho kukakua maeneo ya mapito ya wanayamapori na mipaka ya hifadhi hiyo wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutatua changamoto za uhifadhi mkoani Manyara jana.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...