Kaka na dada wetu,
@imetoshafoundation wa kushirikiana na Umoja wa watu wenye ualbino Tanzania, na Taasisi ya Kansa ya Ocean Road, tumeandaa upimaji wa Kansa kwa watu wenye ualbino waishio jijini Dar es Salaam ikiwa ni jitihada zetu katika kujaribu kupunguza vifo vya watu wenye ualbino vinavyosababishwa na saratani ya ngozi.
Watu wengi hufariki baada ya kugundua ugonjwa ukiwa umwshaenea mwilini, na inawezekana kuutibu ukiwa bado haujafikia hatua mbaya.
Hivyo basi kama unamjua mtu mwenye ualbino umpe taarifa kwamba kuna upimaji wa BURE Ocean Road kwa siku mbili, ili kutambua afya yake na kuanza kupata tiba kabla ugonjwa haujamuathiri.
Sambaza ujumbe, tuokoe maisha
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...