Kumekuwepo na uvumi unaoenezwa kupitia baadhi ya Mitandao ya Kijamii kuwa Idara ya Uhamiaji imetangaza nafasi za ajira kwa nafasi za Mkaguzi Msaidizi, Koplo na Konstebo. Kufuatia kuwepo kwa uvumi huo, Idara ya Uhamiaji inapenda kutoa ufafanuzi kuwa:

1.   Idara haijatangaza nafasi zozote za ajira katika kipindi cha hivi karibuni, hivyo tunawaomba wananchi wasirubuniwe au kushawishiwa na mtu yeyote kutoa kitu chochote ili waweze kusaidiwa kupata kazi Idara ya Uhamiaji kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria na pia hakuna mtu anayeruhusiwa kulipa fedha ili apate ajira katika Idara ya Uhamiaji.

2.   Taarifa za kutangazwa nafasi za kazi zilizotolewa kupitia Mitandao hiyo ya kijamii hazina ukweli wowote, bali ni uzushi uliofanywa na watu au kikundi cha watu kwa malengo wanayoyajua wao.
3.   Idara ya Uhamiaji, kama Taasisi ya Serikali inao utaratibu maalum wa kutangaza nafasi za ajira kwa uwazi kupitia Magazeti, Televisheni na Tovuti yake ambayo ni www.immigration.go.tz
4.   Idara inatoa onyo kwa mtu au watu wanaojihusisha na utoaji wa taarifa za upotoshaji kupitia mitandao ya kijamii, kuhusu huduma za uhamiaji ikiwa ni pamoja na suala la nafasi za ajira. Aidha, Idara haitasita kuwachukulia hatua kali za kisheria wale wote watakao bainika kujihusisha na vitendo hivyo.
  
Imetolewa na;

KITENGO CHA UHUSIANO,

IDARA YA UHAMIAJI
MAKAO MAKUU, DAR ES SALAAM.

01 FEBRUARI, 2018

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...