Na Agness Francis Globu ya jamii
VIONGOZI wa Timu ya Township Rollers inayotarajia kumenyana na mabingwa wa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga SC katika dimba la Uwanja wa Taifa wameamua kufanya ziara jijini Dar es salaam.
Wakizungumza leo, viongozi hao ambao ni Motshegetsi Mafa na Sydney Magagane wamesema lengo la kufanya ziara hiyo ni kuandaa mazingira mazuri ya timu yao sehemu itakapofikia kwa ajili ya mchezo huo na mipango mingine.
Kwa siku ya jana walifika hadi maeneo yaliyopo Makao Makuu ya timu ya Yanga SC eneo la Jangwani jijini Dar es Salaam na kuonana na wenyeji wao ambao ni uongozi wa klabu hiyo na kufanya mazungumzo.
Pia wametembelea Uwanja wa Taifa jijini ambao ndio utakaotumika kwa mtanange huo unaotarajia kupigwa Machi 6 mwaka huu. Timu zote mbili zinashauku ya kusonga mbele kuendelea na michuano hiyo ya Klabu Bingwa Afrika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...