Na David John

WANANCHI wa mtaa wa Bombambili Kata ya Kivule wamepewa somo kuhusu suala zima la upimaji wa ardhi, huku wakielezwa umuhimu wa kurasimisha ardhi yao kwa lengo la kuzifikia huduma mbalimbali za kiserikali

Akizungumza katika mkutano wa wananchi wa mtaa huo ambao uliitishwa na ofisi ya Serikali hiyo. Adolph Milunga ambaye ni mtalaamu mpimaji kutoka chuo cha ardhi mkoani Morogoro aliwaeleza wananchi hao umuhimu wa kupima ardhi na faida Zake.

Amesema hata kuchagua watalaamu kutoka chuo cha Ardhi Morogoro hawajafanya Makosa Kwani ni uhakika kwamba serikali ndio inasimamia ambapo kupimwa kwa ardhi kunakufanya kuondoka kwenye umasikini.

Ameongeza kuwa kupimwa kwa ardhi kunakuwezesha kupata dhamana Mahakamani na mambo mengine kama mirathi. Lakini pia mikopo kwa urahisi tofauti na kuwa na ardhi ambayo haijapimwa.

" wao kama watalaamu wa serikali wanafanya kazi hiyo kwa uadilifu mkubwa mno na kwenye mtaa huu tumetoa ofa ya 160,000 na ofa hii itadumu kwa wiki moja. "alisema . Pia amesema baada ya kumalizika kwa wiki moja hakutakuwa tena kwa maana ahadi tena ya ofa hata hivyo watakwenda kuchungulia na kuona kuna nini kipo huko Benki.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...