Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

 Katibu Mkuu wa Wizara Afya, Jinsia , Wazee na Watoto Dk . Mpoki Lusubisya amesema taaluma ya tiba ya usingizi ni moja ya kiungo muhimu katika matibabu hasa upasuaji katika hospitali zetu.

Dk Mpoki Amesema hayo jijini Dar es Salaam leo alipokuwa akifungua mafunzo ya siku tano kwa wataalamu wa dawa za usingizi kwa hospitali zote zilizopo ukanda wa pwani.

"Kumekuwa na dhana tofauti juu ya tiba ya usingizi kiasi cha watu kuiita ni nusu kaputi jambo ambalo limekuwa likipotosha na kuogopesha wagonjwa hivyo naomba niwaambie kuwa tiba ya usingizi sio nusu kaputi bali ni dawa ya kuzoofisha mishipa"amesema Dk Mpoki.

Amesema kuwa watu wanatakiwa kuwa waelewa zaidi kuwa tiba ya usingizi ni dawa muhimu sana katika kuhakikisha kuwa tiba za upasuaji zinafanikiwa 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dk Mpoki Ulisubisya akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya siku tano ya  awamu ya nne kwa wataalamu wa dawa za usingizi katika hospitali zilizopo katika ukanda wa pwani 
 Mratibu wa Mafunzo ya Wataalamu wa dawa za Usingizi kutoka Tasisi ya Mifupa (MOI), Karima Khalid akizungumza mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya siku tano kwa wataalamu wa dawa za usingizi
 Wataalamu wa Dawa za usingizi wakifatilia kwa makini mafunzo yaliyokuwa yakitolewa na wataalamu wa dawa hizo
Wataalamu wa Dawa za usingizi wakifatilia kwa makini mafunzo yaliyokuwa yakitolewa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...