Kongamano la biashara lililoandaliwa na Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) limefanyika jijini Dar es salaam na kuzungumzia mambo kadha wa kadha hususani fursa katika bomba la mafuta la Tanga hadi Hoima, Huduma za fedha kurahisisha biashara za kimataifa na pia makubaliano ya biashara kati ya TCCIA na Chemba ya biashara kutoka China.
Akizungumza wakati wa kufungua rasmi kongamano hilo Charles Itembe ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Azania alisema “ ikiwa wafanyabiashara watatumia huduma za fedha za kimataifa kama Letter of Credit basi itapunguza utapeli na hivyo kukuza biashara. Pia alielezea jinsi benki ya Azania ilivyo tayari kushirikiana na wafanya biashara katika kukuza biashara na uchumi wa viwanda”Nae Mwenyekiti wa Infotech group Ali Mfuruki aliwaasa wafanya biashara kujenga viwanda vyenye kusaidia lengo la Serikali la kuhakikisha viwanda vinajengwa.
Makamu wa Rais wa TCCIA Octa Mshiu alishukuru wanachama wa TCCIA na waalikwa  kwa kufika na kibadilishana uzoefu na changamo.Mkurugenzi Mtendaji wa EAG Group ambao ndio waandaaji wa kongamano hilo kwa kushirikiana na TCCIA,Imani  Kajula “ alisema mkutano huu ni mwendelezo wa lengo la TCCIA kuwawezesha wanachama wake kuwa na jukwaa la mashauriano.
Wadhamini wa kongamano hilo ni Azania, ATCL na Zurich Insurance.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...