MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Bara, Philipo Mangula amewataka Watanzania kujenga na kuilinda amani nchini na kushangazwa na viongozi wa dini wanaobariki chuki kuwa wanamkosea Mungu.

Pia aliwaonya wanasiasa wanaochochea chuki na kusababisha vurugu na kuwashauri waache kwa kuwa siasa ni uvumilivu na kuumiliana.
Mangula alitoa kauli hiyo jana mjini Musoma alipozungumza na viongozi na wana wana chama wa CCM kwenye ukumbi wa mikutano wa Chama mjini humo.

Alisema kuwa turufu kubwa iliyobaki kwa CCM na watanzania ni amani iliyodumu nchini kwa miaka dahari na hivyo wakati wote wazungumzie taratibu na kutunza amani ya nchi ili kue[uka machafuko vurugu na migogoro inayosababishwa na kuchochewa na wanasiasa.

“Siasa ni kuvumiliana na uvumilivu ndiyo hujenga umoja.Wanasiasa wanapoleta vurugu  wajue wanaoumia ni watoto na wanawake na hivyo tuache chuki tujenge amani ya nchi yetu bila kufanya hivyo hatuwezi kupata maendeleo,”alisema Mangula na kuongeza kuwa;“Nashangaa na kushitushwa na viongozi wa dini wanapojiingiza na kubariki chuki, wanamkosea Mungu.

Machafuko yakishatokea hakuna atakayesalimika kwa kusema mimi ni kiongozi wa dini."Alieleza kuwa kazi ya serikali ni kuwajengea nyumba bali  mazingira mazuri wananchi ili wajijenge na kujifanyia maendeleo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Philipo Mangula akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM wa Mkoa wa Mara jana alipowasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi.Kushoto bi Mwenyekiti wa CCM mkoani Mara Samuel Kiboye Namba Tatu na wa pili kutoka kulia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ( NEC) Mkoa wa Mara Christopher Gachuma. Picha zote na Baltazar Mashaka.
 MWENYEKITI wa CCM Mkoa wa Mara, Samuel Kiboye Namba Tatu (kulia), akizungumza na baadhi ya viongozi na wana CCM waliojitokez kumpokea Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Philipo Mangula wa pili kutoka kushoto.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...