Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Wataalamu wa maswala ya afya wametakiwa kutanua wigo katika Tafiti zao na wajikite zaidi katika tafiti za maradhi yatokanayo na vyanzo vya maji (Water born diseases)

Maradhi hayo ambayo hutokana na maji ikiwemo Kichocho, Matende, Minyoo, Vikope na Malaria huchukua asilimia 60 ya maradhi yanayowasumbua wananchi.

Waziri wa Afya wa Zanzibar Hamad Rashid Mohamed ametoa wito huo alipokuwa akizindua Mpango kazi wa Wataalam wa Malaria kutoka Shirika la Misaada la Marekani na Wizara ya Afya Zanzibar uliofanyika Ukumbi wa Hotel ya Ngalawa mjini Unguja.

Amesema tafiti zitakapofanywa juu ya maradhi hayo zitabainisha chanzo na njia nzuri za kujikinga na mwisho kuifanya Zanzibar kuwa sehemu isiyosumbuliwa na magonjwa hayo.

Waziri Hamad amefahamisha kuwa licha ya Zanzibar kupiga hatua kubwa katika kudhibiti ugonjwa wa malaria bado juhudi zinahitajika za kutokomeza moja kwa moja malaria ifikapo mwaka 2023.
 Naibu Waziri wa Afya Harusi Said Suleiman akitoa salamu zake kabl ya kumkaribisha Waziri wa Afya kufungua mkutano wa Mpango kazi wa Wataalam wa Malaria kutoka Shirika la Misaada la Marekani na Wizara ya Afya Zanzibar uliofanyika Ukumbi wa Hotel ya NGalawa mjini Unguja. Picha na Abdalla Omar-Maelezo Zanzibar.
 Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa Mkutano wa Mpango kazi wa Wataalam wa Malaria kutoka Shirika la Misaada la Marekani na Wizara ya Afya Zanzibar uliofanyika Ukumbi wa Hotel ya NGalawa mjini Unguja. Picha na Abdalla Omar-Maelezo Zanzibar
 Katibu Mkuu Wizara ya Afya Asha Abdulla akitoa neno la shukran kwa Mfuko wa Rais wa Marekani wa kupambana na Malaria (PMI) kwa kuendelea kuiunga mkono Serikali kila hatua. 
 Mkuu wa kitengo cha kupambana na Malaria Zanzibar Dkt. Abdalla Ali akiwasilisha taarifa ya tahmini ya hatua walizozichukua za kupambana na Malaria kwa mwaka 2017 na mikakati yao kwa mwaka huu mbele ya Wajumbe walioshiriki Mkutano wa Mpango kazi wa Wataalam wa Malaria Zanzibar.
Picha ya pamoja

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...