WANACHAMA 3,500 wa Chadema katika Kijiji cha Narakauwo, Kata ya Loiborsiret
Wilayani Simanjiro, wamejiunga na CCM kwa lengo la kumuunga mkono Rais
John Magufuli na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti.
Wananchi
hao ambao awali walikuwa CCM, waliondoka kwenye chama hicho na kujiunga
na Chadema, baada ya kigogo mmoja kukata majina ya baadhi ya wagombea
waliokuwa wanawaunga mkono kwenye Kijiji hicho na kata hiyo mwaka 2015.
Akizungumza
jana wakati akiwapokea wanachama hao wapya kwenye mkutano uliofanyika
kijiji cha Narakauwo, Mnyeti ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya siasa ya
CCM Mkoani Manyara, alitoa onyo kwa wanasiasa wanaowayumbisha wananchi
wa eneo hilo.
Mnyeti
alisema kuna baadhi ya viongozi wa wilaya hiyo bado wamelala kwani
wanadhani huu ni wakati wa kufanya siasa ili hali ilishakwisha mwaka
2015 na huu ni wakati wa kufanya kazi. "Kuna
baadhi ya viongozi walikaa vikao usiku ili kukwamisha suala hili,
nawapa onyo la mwisho, kama kuna mtu anataka ubunge asubiri mwaka 2020
siyo leo," alisema Mnyeti.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti akizungumza na wananchi wa kijiji cha Narakauwo Wilayani Simanjiro juu ya mgogoro wa uongozi na kumuagiza mkuu wa Wilaya hiyo mhandisi Zephania Chaula aitishe kikao cha wanakijiji hao ili kujadili tatizo lao.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...