Na Tiganya Vincent
WAKANDARASI Kitanzania wametakiwa kuzingatia ubora, viwango  vya kazi zao ili waweze kuaminika kwa Serikali na hivyo kupata fursa kubwa ya kupewa miradi mipya inayotarajiwa kujengwa hapa nchini.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri wakati alipokutana na ujumbe wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi(CRB)

Alisema ujenzi wa miradi chini ya kiwango na ambayo haidumu kwa muda mrefu kutawasababisha kutopewa kipaumbele pindi miradi inapokuwa ikitangazwa na badala yake miradi hiyo kutekelezw na wakandarasi wa kigeni.

Mwanri alisema ni vema wajenga tabia ya kushirikiana katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ili waweze kuwa na nguvu kubwa na vifaa vingi ambavyo ndivyo vitawasaidia kuikamisha kwa wakati na kwa kiwango bora kinachotakiwa.

Alisema matokeo mazuri ya utekelezaji wa miradi yataifanya Serikali kutoa kipaumbele kwa Kampuni za Watanzania katika miradi ya ujenzi , jambo ambalo litawasaidia kujiimarisha zaidi.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri(kulia) akiagana jana na Meneja wa Wakala wa Barabarani Tanzania(TANROADS) Mkoani humo, Damian Ndabalinze (kushoto) mara baada ya mazungumzo yaliyolenga kujua hali ya ukarabati wa barabara zilizoharibiwa na mvua iliyonyesha hivi karibuni na kusababisha kukatika kwa mawasilano katika njia mbalimbali.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri(kulia) akitoa maagizo jana kwa Mfanyakazi katika Kitalu cha Miche ya Miti mbalimbali cha Manispaa ya Tabora, Mariam Christopher(kushoto) na Meneja wa Wakala wa Mistu Tanzania (TFS) Manispaa ya Tabora Bakilana Mashauri (katikati) kuhusu kuotesha miti maji mingi kwa ajili ya kupanda katika maeneo mbalimbali katika Manispaa hiyo.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri(kulia) akitoa maagizo jana kwa Meneja wa Wakala wa Mistu Tanzania (TFS) Manispaa ya Tabora, Bakilana Mashauri (kulia) kuhusu kuotesha miti maji mingi kwa ajili ya kupanda katika maeneo mbalimbali katika Manispaa hiyo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...