Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) imeahidi kuimarisha taaluma ya Maendeleo ya Jamii ili iweze kuongeza tija katika jamii. 

Hayo yamesemwa mjini Morogoro na Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia Vyuo vya Maendeleo ya Jamii Bi. Neema Ndoboka wakati wa kikao cha wadau waliokutana kujadili rasimu ya mitaala na kupata maoni yatakayowezesha kuboresha mitaala ya vyuo hivyo.

Bi. Neema amesema kuwa Wizara itafuatilia kwa karibu utoaji mafunzo ya fani ya Maendeleo ya Jamii kwa vyuo vyake inavyovisimamia na pia kushirikiana na Mamlaka nyingine katika kufuatilia utoaji wa mafunzo hayo kwa Vyuo visivyosimamiwa na Wizara. 

“Kikao cha wadau cha kupitia mitaala ya vyuo vya maendeleo ya jamii kinajenga uwezo wa Wizara katika kuhakikisha usimamizi wa vyuo hivi unazingatia Kanuni na taratibu za Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) jukumu ambalo Wizara imekuwa ikilitekeleza kila inapohitajika” alisisitiza Bi Neema. 

Akizungumza katika mkutano huo Kaimu Mkuu wa Tasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru Dkt. Bakari George suala la kuwa na mkutano wa wadau kupitia rasimu ya mitaala ya vyuo vya Maendeleo ya Jamii ni hitaji la muhimu ili kupta maoni ya takayosaidia kkuboresha mada, mahudhui, mbinu, stadi za kufundishia na kujifunzia na maarifa.
 Mkurugenzi Msaidizi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anayesimamia Vyuo vya Maendeleo ya Jamii,  Neema Ndoboka akieleza mpango wa Wizara katika kusimamia Sekta ya Maendeleo ya Jamii kupitia Vyuo vya Maendeleo ya Jamii wakati akifungua Kikao cha wadau wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii kujadili Rasimu ya Mitaala ya fani ya Maendeleo ya Jamii kilichofanyika Mjini Morogoro Kushoto ni Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru Dkt. Bakari George.
 Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru, Dkt. Bakari George akieleza dhumuni la kikao cha kupitia Rasimu ya Mitaala ya Fani ya Maendeleo ya Jamii  kupitia Vyuo vya Maendeleo ya Jamii  wakati wa Kikao hicho cha wadau wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii kujadili Rasimu ya Mitaala ya fani ya Maendeleo ya Jamii kilichofanyika Mjini Morogoro.
 Afisa Maendeleo ya Jamii, Bw. Abel Palala akiwasilisha mada kuhusu Mtaala wa mafunzo ya Maendeleo ya Jamii ngazi ya Stashahada katika  kikao cha kupitia Rasimu ya Mitaala ya Fani ya Maendeleo ya Jamii  katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii wakati wa Kikao hicho cha wadau wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii waliokutana kujadili Mitaala pendekezi ya fani ya Maendeleo ya Jamii katika ukumbi wa TAFOLI Mjini Morogoro.
 Mhadhiri wa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru, Simon Kilasala akitoa taarifa  ya utafiti wa Soko la ajira kwa wataalam wa Maendeleo ya Jamiki wakati wa  kikao cha  kupitia Rasimu ya Mitaala ya Fani ya Maendeleo ya Jamii  kupitia Vyuo vya Maendeleo ya Jamii wakati wa Kikao hicho cha wadau wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii wanaokutana kujadili Rasimu ya Mitaala ya fani ya Maendeleo ya Jamii katika ukumbi wa TAFOLI Mjini Morogoro.
 Mkufunzi Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba, Kidubya Kulamiwa akiwasilisha mada kuhusu Mtaala wa mafunzo ya Maendeleo ya Jamii ngazi ya Astashahada katika  kikao cha kupitia Rasimu ya Mitaala ya Fani ya Maendeleo ya Jamii  katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii wakati wa Kikao hicho cha siku moja cha wadau wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii waliokutana kujadili Rasimu ya Mitaala ya fani ya Maendeleo ya Jamii kilichofanyika Mjini Morogoro.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...