Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(TUCTA) limesema
litatumia kongamano la Siku ya wanawake linalotarajiwa kufanyika
kesho  kujadili nafasi ya mwanamke na namna ya kutatua changamoto
zinazowakabili maeneo ya kazi.

Akizungumza jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake wa TUCTA,
Rehema Ludaga amesema kongamano litafanyika jijini Dar es Salaam
ikiwa ni siku moja kabla ya kilele cha Siku ya Wanawake Duniani
ambayo ni Machi 8 ya kila mwaka.

"Tutatumia kongamano letu la Machi 7(kesho) kujadili mambo
mbalimbali yanayowakabili wanawake kwenye maeneo ya kazi na moja
ya mjadala utahusu namna ya kuangalia changamoto zilizopo na  nini
kifanyike kukabiliana nazo au kuziondoa kabisa"amesema Ludaga.

Kuhusu kauli mbiu ya mwaka huu kwenye maadhimisho ya siku ya
mwanamke duniani inasema hivi "Tathimini ya Unyanyasaji wa kijinsia
mahala pakazi".

Kwa upande wa Katibu Mkuu wa TUCTA, Dk.Yahya Msigwa amesema
kila mwaka wanafanya kongamano ila kupata mawazo ya wanawake
kwa lengo la kuboresha mahali pakazi na mgeni rasmi kwenye
kongamano anatarajiwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala Dar es Salaam
Sophia Mjema.
Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Rehema Ludaga akizungumza kuhusiana na Kongamano siku ya wanawake, jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa TUCTA, Dk. Yahya Msigwa akizungumza na kuhusiana na utaratibu wa TUCTA kuandaa kongamano la wanawake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...