Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akimkabidhi mmoja wa wafanyabiashara kitambulisho na Namba ya Utambulisho ya Mlipakodi (TIN) wakati wa uzinduzi wa zoezi la utoaji vitambulisho Dar es Salaam Machi 27, 2018. Pamoja naye ni Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA), Charles Kichere (mwenye miwani) na viongozi waandamizi wa Mamlaka hiyo. 
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA), Charles Kichere (wa pili kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema wakipata maelezo kutoka kwa Afisa wa Kodi, Dina Kaka jinsi ya kuandaa risiti ya kitambulisho cha Mfanyabiashara wakati wa uzinduzi wa zoezi la utoaji vitambulisho.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA), Charles Kichere akimkabidhi Mfanyabiashara Mshamu Nakukwa kitambulisho wakati wa uzinduzi wa zoezi la utoaji vitambulisho Dar es Salaam Machi 27, 2018.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...