Takribani
kiasi cha Shilingi Milioni 140 zimepatikana katika kipindi cha miaka
miwili iliyopita baada ya Wananchi wanaopata huduma za Mpango wa
Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa
Maendeleo ya Jamii –TASAF- katika Wilaya ya Chato Mkoani Geita kujiunga
na Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii-CHF.
Mkuu wa Wilaya ya Chato Bw.Shaaban Ntarambe amewambia Wandishi wa Habari wanaotembelea Mkoani Geita kuona namna Wananchi wanaonufaika na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wanaovyotumia fursa hiyo kuwa pamoja na kuanzisha shughuli za kiuchumi ,walengwa hao pia wamehamasishwa kujiunga na CHF kwa kuchangia kiasi cha shilingi 10,000 kwa mwaka na kupata huduma za matibabu kwa kipindi chote cha mwaka.
Amesema kumekuwa na mwitikio mzuri kwa Walengwa hao wa TASAF kujiunga na huduma za CHF kwa kutumia sehemu ya ruzuku wanayoipata kupitia utaratibu wa uhawilishaji fedha na hivyo kuboresha afya zao na kupunguzia mzigo wa serikali kuwahudumia hususani pale wanapohitaji huduma ya matibabu.
Kwa Upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Chato Dr Athanus Ngambakubi amesema katika vijiji ambavyo TASAF inatoa huduma kwa Kaya Maskini ambazo zimejiunga na CHF,Wataalam wa Afya hawalazimiki kutumia nguvu kubwa kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kupata huduma za matibabu hospitalini kinyume na ilivyokuwa kabla ya kuanza kwa Mpango huo.

Mmoja wa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na TASAF ,Esther Seleman mkazi wa kijiji cha Mabalasana katika halmashauri ya wilaya ya Geita akiwaonyesha Waandishi wa Habari (hawapo pichani) shamba la Mpunga ambalo amelima kwa kutumia sehemu ya ruzuku aliyoipata kupitia utaratibu wa uhawilishaji fedha kama njia mojawapo ya kujiongezea kipato.
Mmoja wa Walengwa wa TASAF katika kijiji cha Isamilo katika halmashauri ya wilaya ya Geita akiwa katika shughuli ya kushona nguo kwa kutumia cherahani alichokinunua baada ya kudunduliza fedha za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kama njia ya kujiongezea kipato.
Mmoja wa Walengwa wa TASAF katika kijiji cha Mabalasana katika halmashauri ya wilaya ya Geita akiwa mbele ya nyumba na matofari aliyopata kwa kutumia fedha za Mpango wa kunusuru Kaya Maskini katika jitihada za kuboresha makazi yake.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Geita.Ali Kidwaka akizungumza na Wandishi wa Habari juu ya utekelezaji wa Shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF hususani Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika halmashauri yake ambapo amesema Mpango huo umekuwa chachu ya kaya za Walengwa kupiga vita umaskini kwa mafanikio makubwa na kutoa wito wa kutekeleza Mpango huo katika vijiji vyote.
Mmoja wa Walengwa wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF ,BI. Sabina Mtangwa (aliyevaa gauni jekundu ) mkazi wa kijiji cha Isamilo katika halmashauri ya wilaya ya Geita ,akimwonyesha Afisa Mawasiliano wa TASAF Estom Sanga mbuzi na ng’ombe waliozaliana baada ya kununua mbuzi na kuwauza aliowapata kwa kutumia fedha za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini.
Mkuu wa Wilaya ya Chato Bw.Shaaban Ntarambe amewambia Wandishi wa Habari wanaotembelea Mkoani Geita kuona namna Wananchi wanaonufaika na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wanaovyotumia fursa hiyo kuwa pamoja na kuanzisha shughuli za kiuchumi ,walengwa hao pia wamehamasishwa kujiunga na CHF kwa kuchangia kiasi cha shilingi 10,000 kwa mwaka na kupata huduma za matibabu kwa kipindi chote cha mwaka.
Amesema kumekuwa na mwitikio mzuri kwa Walengwa hao wa TASAF kujiunga na huduma za CHF kwa kutumia sehemu ya ruzuku wanayoipata kupitia utaratibu wa uhawilishaji fedha na hivyo kuboresha afya zao na kupunguzia mzigo wa serikali kuwahudumia hususani pale wanapohitaji huduma ya matibabu.
Kwa Upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Chato Dr Athanus Ngambakubi amesema katika vijiji ambavyo TASAF inatoa huduma kwa Kaya Maskini ambazo zimejiunga na CHF,Wataalam wa Afya hawalazimiki kutumia nguvu kubwa kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kupata huduma za matibabu hospitalini kinyume na ilivyokuwa kabla ya kuanza kwa Mpango huo.

Mmoja wa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na TASAF ,Esther Seleman mkazi wa kijiji cha Mabalasana katika halmashauri ya wilaya ya Geita akiwaonyesha Waandishi wa Habari (hawapo pichani) shamba la Mpunga ambalo amelima kwa kutumia sehemu ya ruzuku aliyoipata kupitia utaratibu wa uhawilishaji fedha kama njia mojawapo ya kujiongezea kipato.

Mmoja wa Walengwa wa TASAF katika kijiji cha Isamilo katika halmashauri ya wilaya ya Geita akiwa katika shughuli ya kushona nguo kwa kutumia cherahani alichokinunua baada ya kudunduliza fedha za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kama njia ya kujiongezea kipato.

Mmoja wa Walengwa wa TASAF katika kijiji cha Mabalasana katika halmashauri ya wilaya ya Geita akiwa mbele ya nyumba na matofari aliyopata kwa kutumia fedha za Mpango wa kunusuru Kaya Maskini katika jitihada za kuboresha makazi yake.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Geita.Ali Kidwaka akizungumza na Wandishi wa Habari juu ya utekelezaji wa Shughuli za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF hususani Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika halmashauri yake ambapo amesema Mpango huo umekuwa chachu ya kaya za Walengwa kupiga vita umaskini kwa mafanikio makubwa na kutoa wito wa kutekeleza Mpango huo katika vijiji vyote.

Mmoja wa Walengwa wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF ,BI. Sabina Mtangwa (aliyevaa gauni jekundu ) mkazi wa kijiji cha Isamilo katika halmashauri ya wilaya ya Geita ,akimwonyesha Afisa Mawasiliano wa TASAF Estom Sanga mbuzi na ng’ombe waliozaliana baada ya kununua mbuzi na kuwauza aliowapata kwa kutumia fedha za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...