Na Sophia Mtakasimba (TaSUBa).

Mchezo wa kuigiza wa jukwaani unaofahamika kwa jina la Afrika zinduka, umetikisa tamasha la kumi la kigoda cha Mwalimu Nyerere lililoendelea  katika ukumbi wa Nkuruma wa chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Mchezo huo uliobeba ujumbe wa namna  Bara la Afrika linavyoteseka na umasikini mkubwa ile hali  lina utajiri mkubwa wa mali asili , ardhi na madini umetungwa , umeongozwa na kuchezwa na Kikundi cha “Bagamoyo Players” cha Taasisi ya Sanaa na utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ili kuchagiza ujumbe wa tamasha la mwaka huu uliosema “wimbi la uporaji wa rasilimali Afrika wanyonge wanajikwamuaje”

Akizungumza katika siku ya pili ya Tamasha hilo Mwenyekiti wa Kigoda cha Taaluma cha mwalimu Nyerere, Profesa Penina Mlama , amesema kuwa igizo hilo limeakisi namna halisi ya maisha ya sasa ya muafrika hivyo ni wakati wa kuzinduka.

“Wenzetu wa TaSUBa wametuambia Afrika Zinduka ,sasa huu ndio wakati wetu wa kuzinduka na kuona namna Afrika inaweza kunufaika na rasilimali zake.” Alisema bi Mlama

Tamasha la kigoda cha kitaaluma cha Mwl,nyerere  ambalo kwa mwaka huu limetimiza miaka kumi toka kuanzishwa kwake limefanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 11-13 Aprili  ambapo mada mbalimbali kuhusu masuala ya kijamii zimejadiliwa .
 Wasanii wa kikundi cha Bagamoyo Players cha TaSUBa wakionesha igizo la Afrika Zinduka katika tamasha la kumi la kigoda cha mwalimu Nyerere.
 Wasanii wa kikundi cha Bagamoyo Players cha TaSUBa wakionesha igizo la Afrika Zinduka katika tamasha la kumi la kigoda cha mwalimu Nyerere.
Wasanii wa kikundi cha Bagamoyo Players cha TaSUBa wakionesha igizo la Afrika Zinduka katika tamasha la kumi la kigoda cha mwalimu Nyerere.
washiriki wa tamasha wakifuatilia igizo la Afrika Zinduka

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...