Na.Vero Ignatus ,Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pohn Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa nyumba za polisi na vituo vya polisi Jijini Arusha.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa polisi jijini hapa DCP Charles Mkumbo amesema kuwa kutakuwa na uzinduzi wa vituo viwili cha Utalii na Diplomasia na kingine ni Kituo cha daraja la kati kilichopo Murieti Jijini Arusha.
Kamanda Mkumbo amesema kuwa kutakuwepo pia na maonyesho mbalimbali ya Jeshi la Polisi linavyofanya kazi za kuwahudumia wananchi ambapo maonesho hayo yatafanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid .
Amewataka wananchi kutokuwa na hofu kwani hali ya usalama Jijini hapa umeimarishwa na amewaomba wajitokeze kwa wingi katika sherehe hizo.
Kituo chaPolisi cha Utalii na Diplomasia kinachotarajiwa kuzinduliwa April 7 Jijini Arusha.Picha na Vero Ignatus Blog.

Baadhi ya Nyumba za Polisi zinazotarajiwa kuzinduliwa na Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pohn Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa nyumba za polisi na vituo vya polisi Jijini Arusha.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa polisi jijini hapa DCP Charles Mkumbo amesema kuwa kutakuwa na uzinduzi wa vituo viwili cha Utalii na Diplomasia na kingine ni Kituo cha daraja la kati kilichopo Murieti Jijini Arusha.
Kamanda Mkumbo amesema kuwa kutakuwepo pia na maonyesho mbalimbali ya Jeshi la Polisi linavyofanya kazi za kuwahudumia wananchi ambapo maonesho hayo yatafanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid .
Amewataka wananchi kutokuwa na hofu kwani hali ya usalama Jijini hapa umeimarishwa na amewaomba wajitokeze kwa wingi katika sherehe hizo.

Kituo chaPolisi cha Utalii na Diplomasia kinachotarajiwa kuzinduliwa April 7 Jijini Arusha.Picha na Vero Ignatus Blog.


Baadhi ya Nyumba za Polisi zinazotarajiwa kuzinduliwa na Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...