Katika kutekeleza Sera ya Diplomasia ya Uchumi, Ubalozi wa Tanzania
nchini Uholanzi kwa kushirikiana na Taasisi ya Wafanyabiashara ya
Uholanzi (Dutch Council for International Business - DCIB) na Kituo cha
Uwekezaji Tanzania (TIC) zimeandaa Warsha ya Biashara na Uwekezaji
iliyofanyika jijini The Hague nchini Uholanzi tarehe 29/03/2018.
Lengo kuu la Warsha hiyo, pamoja na kuendeleza na kukuza uhusiano mzuri
uliopo kati ya Tanzania na Uholanzi, ni kutangaza fursa mbalimbali za
biashara na uwekezaji zilizopo nchini Tanzania hususan katika Sekta za
Viwanda, Ufugaji, Uvuvi, Utalii, Ujenzi, Kilimo na Miundombinu ya Kilimo.
Aidha, Warsha hiyo iliyohudhuriwa na Wawakilishi wa Makampuni takriban
sitini (60) ni mwendelezo na jitihada mbalimbali ambazo Kituo cha
Uwekezaji Tanzania kwa kushirikiana na Balozi za Tanzania zilizopo nje ya
nchi kuendeleza diplomasia ya uchumi ili kuweza kukuza uchumi wa
Tanzania na kufikia malengo ya Serikali kuwa nchi ya uchumi wa kati na
uchumi wa viwanda.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
nchini Uholanzi, Irene Kasyanju, akitoa neno la ukaribisho wakati wa Warsha ya Biashara na
Uwekezaji.
Baadhi ya washiriki waliohudhuria Warsha ya Biashara na Uwekezaji Jijini The
Hague wakimsikiliza Mhe. Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. Geoffrey I. Mwambe
akitoa mada kwa wahusika wa Makampuni mbalimbali kutoka Uholanzi waliohudhuria
Warsha hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...