Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (mwenye suti ya bluu kulia), leo akiteta
jambo na Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya
Uingereza, Bw. Matthew Rycroft mara baada ya kukamilika kwa zoezi la mbwa
wa polisi kuonesha namna wanavyokamata dawa za kulevyia na nyara za
serikali katika mizigo ya abiria kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha
Julius Nyerere (JNIA).
Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius
Nyerere (JNIA), Bw. Paul Rwegasha (kulia) akiongea na Kaimu Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard
Mayongela baada ya zoezi la mbwa kuonesha namna wanavyobaini mizigo
yenye nyara za serikali na dawa za kulevyia leo kiwanjani hapo.
Koplo Chesco Mbise akimwongoza mbwa anayeitwa Max-Z kuondoka mara baada ya zoezi la kuonesha namna anavyokamata dawa za kulevyia katika mizigo ya abiria kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), ambapo leo Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya Uingereza (hayupo pichani) alipotembelea na kuona zoezi hilo. Mbwa huyu ni kati ya wawili waliotolewa kwa msaada na serikali ya Marekani.
Askari Hadson Muhuma akiwa amemshika mbwa anayeitwa Nopi wakati akifanya zoezi la kutambua mizigo ya abiria yenye nyara za serikali zikiwemo pembe za Ndovu, lililofanyika leo kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), baada ya kutembelewa na Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Serikali ya Uingereza (hayupo pichani).
Katibu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya
Serikali ya Uingereza, Bw. Matthew Rycroft (wapili kushoto) akiwa na Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw.
Richard Mayongela (wa pili kulia) wakimsikiliza Bw. Matt Jenkins (aliyekaa),
ambaye ni Afisa wa UK Border Force wa Kitengo cha dawa za kulevyia katika
Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA). (Picha zote na
Bahati Mollel wa TAA).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...