Na Mwandishi wetu, Dodoma
WAANDISHI wa habari wanapaswa kuandika na kutangaza habari zao kwa weledi na kuzingatia maadili ili kuepuka kuandika habari zinazoipa serikali sababu ya kufungia vyombo vyao.
Kauli hiyo imetolewa mwandishi wa habari mkongwe nchini Tanzania Bw. Ndimara Tegambwage wakati akitoa mada ya uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania kwenye kongamano la maadhimisho ya siku ya Uhuru Wa Vyombo vya Habari Duniani ambayo nchini Tanzania yanafanyika kitaifa mkoani Dodoma.
Kila Mei 2-3 kila mwaka ni siku za kimataifa ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani.
Aidha katika mada yake hiyo Ndimara alisema Serikali barani Afrika zimekuwa zikikosa uvumilivu na kunyima uhuru vyombo vya habari licha ya kuwa uhuru huo unatambuliwa na katiba za mataifa ya Afrika.
Bw. Ndimara amebainisha kuwa, wakati serikali za Africa zikitoa haki ya kusajili vyombo vya habari hususani Radio, Runinga na Magazeti, serikali zinapokosolewa huvifungia vyombo hivyo kwa tuhuma za kukiuka maadili jambo ambalo alidai kuwa si la ukweli.
Mkongwe huyo wa tasnia ya habari nchini Tanzania amebainisha kuwa serikali nyingi barani Afrika zimekosa uvumilivu na kutumia nguvu nyingi kunyamanzisha wanahabari.
Huku akinukuu hotuba ya Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai ambaye ameonya kuwepo kwa wananchi wanaotumia mitandao ya kijamii vibaya aliwataka waandishi wa habari kuwa makini kutokana na sheria mbalimbali zinazowazunguka zinaohitaji weledi wa hali ya juu katika kuhabarisha.
Awali akitoa hotuba ya ufunguzi wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini Tanzania, Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai amesema Tanzania inautambua mchango wa vyombo vya habari katika kurahisisha mawasiliano ya jamii na kuharakisha maendeleo lakini inakwazwa na kuwepo kwa baadhi ya vyombo vya habari na wanahabari ambao huandika habari nyingi za kutungwa na za uongozi.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai akifungua kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit akitoa salamu za Unesco wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari nchini (UTPC), Jane Mihanji akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai kufungua kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo akizungumzia malengo ya maendeleo endelevu na jukumu la waandishi wa habari kutumia nafasi zao kutoa taarifa kuhusu malengo hayo kwa jamii ili yatekelezeke kwa urahisi, katika kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mtaalamu wa Masuala ya Vyombo vya Habari na Mkufunzi wa kujitegemea, Rose Haji Mwalimu akiongoza mjadala kuhusu mada: Wajibu wa Uongozi, Vyombo vya Habari na Sheria katika kuhakikisha haki inatendeka na kuonekana inatendeka wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Mwandishi wa Habari Nguli, Ndimara Tegambwage na mwezeshaji wa mada inayohusu; Wajibu wa Uongozi, Vyombo vya Habari na Sheria katika kuhakikisha haki inatendeka na kuonekana inatendeka: wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Wakili na Mwandishi wa Habari ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya MISA-TAN, James Marenga akichangia mada wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Nashera jijini Dodoma.
 Mdau wa Habari Ernest Sungura akishiriki kuchangia maoni katika mjadala uliowasilishwa na mwandishi nguli Ndimara Tegambwage (hayupo pichani) wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Habari Unesco nchini, Nancy Kaizilege (kulia) na Mshauri wa Utawala Bora na Haki za Binadamu wa Ubalozi wa Sweden nchini, Anette Widholm Bolme wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Pichani juu na chini Sehemu ya washiriki ambao ni wahariri, waandishi wa habari, wadau wa tasnia ya habari na wageni waalikwa waliohudhuria kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wakiwemo wahariri, wadau wa habari na waandishi wa habari waliohudhuria kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa habari na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, Ubalozi wa Umoja wa Ulaya pamoja na wamiliki wa vyombo vya habari vya kijamii waliohudhuria kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...