Na Emmanel Massaka ,Globu ya jamii

MWENYEKITI wa Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam Said Subety amewataka madereva wote wa gari, pikipiki na bajaji kuwa makini katika Sikukuu ya Eid Alfitri kwani siku hiyo kunakuwa na watoto wengi barabarani.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Subety amesema katika Sikuu ya Eid ni vema jamii ikachukua tahadhari kwa kuhakikisha hakuna ajali ambazo zinatokea na hasa kwa watoto na kwamba vipengele vya umakini vimegawanyika katika maeneo matatu katika sherehe ya sikuku hiyo. 

Amesema kwanza ni umakini kwa wazazi na walezi ambapo amefafanua jinsi watoto wanavyokuwa wengi wakisheherekea sikuku hiyo kwa kurandaranda sehemu mbalimbali wakiwa na furaha na hata bila ya tahadhari yoyote, bila wazazi au uangalizi makini wanahitaji kuangaliwa kwa umakini.

Amesema na mara nyingi kiongozi wao ni mtoto mwenzao na hakika matembezi yao wanatembelea sehemu nyingine ni hatarishi kama baharini ambako watoto wengi hupenda kwenda huko kwa ajili ya kuogelea na barabarani, hivyo amewasisitiza wazazi wasiwaache watoto wakienda bila uangalizi wa maana.

Pia kwa wenye kumbi za starehe ambazo zitachukua watoto washeherekee nao wawe makini na wasifanye biashara kwa tamaa kubwa kwa kuwajaza watoto kupita uwezo wa kumbi zao kwani ni hatari.

"Tunawapongeza sana Waislamu wote hususani wale waliofunga Mwezi mtukufu wa Ramadhani. Mwenyezi Mungu apokee swaumu zetu, kwa baraka za funga zao, Mungu atujalie ulinzi wa amani wa nchi yetu, Rais wetu Dk. John Magufuli na wananchi wote, Amen,"amesema. 
 Mjumbe wa kamati ya utekelezaji baraza la Wilaya ya Wazazi Kinondoni,kwege Nyangunda asisitiza jambo katika mkutano huo uliofanyika katika ofisi za sisi Kinondoni.
 Mwenyekiti wa Wazazi Wilaya ya Kinondoni wa Chama cha Mapinduzi,Said Dubety (kulia)akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Mandereva waendeshai vyombo vya moto kuwa makini barabarani,siku ya sikukuu ya (Eid Elfri) .kulia ni Mjumbe wa mkutano mkuu wazazi Taifa,Hassan Kaniki.(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii)
Picha ya pamoja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...