Na Humphrey
Shao, Globu ya Jamii
Mkuu wa mkoa
wa Geita,Mhandisi Robert Gabriel amewataka Vijana kuendelea kuwa wabunifu kwa
kutumia teknolojia ya Ict ili waweze kuleta tija katika mapinduzi ya uchumi wa
Viwanda.
RC Gabriel
amesema hayo mapema leo jijini Dar es Salaam alipotembelea banda la Chuo Cha Kumbukumbu
ya Mwalimu Nyerere lililopo katika Maonesho ya 42 ya Sabasaba Jijini Dar es
Salaam na kujionea ubunifu wa umwagiliaji maji shambani kwa kutumia teknolojia ya mfumo wa TEHAMA uliofanywa na Wanafunzi wa Chuo hicho.
“nahitaji
kuona project hii ikihamishiwa katika shamba kubwa la ekari tano, na mimi niko
tayari kutumia teknolojia hii katika mkoa wangu wa Geita ili kusaidia Kilimo
cha umwagiliaji” amesema Rc Gabriel.
Rc Gabriel
aliendelea kwa kukipongeza Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kwa kuendelea kuwa wabunifu na
kusimamia fikra za Mwasisi wan chi hii Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel akieleza jambo mara baada ya kupokea maelezo juu ya mradi wa umwagiliaji maji shambani kwa kutumia TEHAMA.
Mmoja wa wafanyakazi wa Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere akitoa maelezo kuhusiana na programu za chuo kwa Wananchi waliotembelea banda hilo.
Mhadhiri wa Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere , Samwel Lunyelele akitoa maelezo kwa wakazi wa Jijini Dar es Salaam waliotmebela banda la chuo hicho katika Maonesho ya 42 ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam
Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliotembelea Banda la Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere wakiangalia historia ya chuo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...