SHIRIKA la Haki Madini la jijini Arusha, limewajengea uwezo viongozi wa serikalini, wa kimila na baadhi ya wananchi wa mikoa ya kanda ya kaskazini, juu ya utambuzi wa uthamini wa fidia ya ardhi na madini. 

Mwanasheria wa shirika la Haki Madini, Erick Luwogo akizungumza mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro,  alisema kupitia mafunzo waliyotoa, elimu ya fidia ya ardhi na madini itaifikia jamii ipasavyo. 

Luwogo alisema wanataka kuona changamoto ya ucheleweshaji wa fidia, isiyo sahihi na kukatazwa kufanya maendelezo zinapatiwa ufumbuzi kwa haraka. 

"Tumekutanisha wadau wengi wakiwemo wanasheria, wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji, viongozi wa kimila, jamii na lengo hasa ni kupata majawabu ili serikali inapotoa fidia iwe inafanya kwa wakati," alisema. 

Mkazi wa mji mdogo wa Mirerani, Anthony Mavili alisema miradi mingi mikubwa ya eneo hilo imefanyika lakini wananchi ambao waliathirika kwa namna moja au nyingine hawakufidiwa. 
 Baadhi ya viongozi wa serikali, wanasheria na wananchi walioshiriki kwenye warsha ya sheria ya fidia ya ardhi na madini iliyoandaliwa na shirika la Haki Madini, mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro. 
 Baadhi ya walioshiriki warsha hiyo mwanasheria wa TLS Linda Shamba (kushoto) na mhandisi wa madini Ernest Sanka.
 Mmoja kati ya wawezeshaji wa warsha hiyo, mthamini mkuu wa Halmashauri ya jiji la Arusha, Rosemary Kirenga (kushoto) na mwanasheria wa shirika la Haki Madini, Erick Luwogo wakizungumza na washiriki wa warsha hiyo. 
Mkazi wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Anthony Mavili akizungumza juu ya fidia kwenye warsha ya sheria ya fidia ya ardhi na madini iliyoandaliwa na shirika la Haki Madini mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...