Taasisi
isiyo ya Kiserikali ya Women at Web Tanzania imezindua mradi maalumu
wenye lengo la kutoa mafunzo ya matumizi ya mitandao ili kuongeza uwepo
wa kundi hili mitandaoni.
Mradi huo unaofadhiliwa na Shirika la DW Akademie la nchini Ujerumani una lengo la kuhamasisha matumizi bora ya mitandao ikiwamo kuongeza mijadala ya maendeleo kwa wanawake katika mitandao.
Mradi huo unaofadhiliwa na Shirika la DW Akademie la nchini Ujerumani una lengo la kuhamasisha matumizi bora ya mitandao ikiwamo kuongeza mijadala ya maendeleo kwa wanawake katika mitandao.

Akizungumza
wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi huo iliyofanyika leo jijini Dar es
Salaam, mmoja wa viongozi wa mradi huo Carol Ndosi amesema kwamba moja
ya shughuli zitakazofanyika katika uhamasishaji huo ni mafunzo kwa
wanawake yanayohusu njia za kujilinda na vurugu za mitandao, kutambua
fursa zilizopo mitandaoni pamoja na mambo mengine.
Alisema kuwa kwa sasa Tanzania hakuna takwimu zilizo wazi za udhalilishaji wa wanawake kwenye mitandao japokuwa wengi waliopo wameshakutana na aina ya udhalilishaji kwenye mitandao, hasa ya kijamii.

“Idadi
ya watu wanaomiliki smart phone inaongezeka hivyo kuongeza hatari za
wanawake kuwa wahanga wa unyanyasi katika platform hizo, kwa hiyo
kupitia mradi huu, pamoja na kuhamasisha wanawake kuongezeka kutumia hii
mitandao, tutawapatia mafunzo ya namna ya kujilinda ama kutambua wale
wanataka kuwafanyia ukatili.
“Lengo letu ni kuhakikisha kuwa kwa kuwa bado tuna ‘gap’ kubwa sana la wanawake kushiriki katika mijadala ya maendeleo nje ya mitandao, basi watumie fursa za mitandao kushiriki mijadala hiyo na kujiletea maendeleo,” alisema Ndosi.
“Lengo letu ni kuhakikisha kuwa kwa kuwa bado tuna ‘gap’ kubwa sana la wanawake kushiriki katika mijadala ya maendeleo nje ya mitandao, basi watumie fursa za mitandao kushiriki mijadala hiyo na kujiletea maendeleo,” alisema Ndosi.

Kwa kuanzia, mradi huo utaendesha mafunzo katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na pia kwa upande wa Zanzibar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...