Na Agness Francis,Globu ya Jamii
Kampuni ya burudani ya Isbah entertainment imedhamiria  kuwainua wasanii wa muziki wa kiasili   aina ya mnanda,vanga,mdundiko pamoja na segere ambao wamesahaulika kwa muda mrefu.

Katika kuwasaidia wanamuziki hao pamoja na kurejesha heshima ya muziki huo kwa jamii,  kampuni hiyo imeandaa tamasha kubwa  litakalotambulika kwa jina la Wakwetu Festival wakiwa na kauli mbiu isemayo  Vumbi tu.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi zao Mratibu wa tamasha hilo Yakub Sadik amesema kuwa lengo la kuandaa shoo hiyo ni kutaka kuwapa nguvu wasanii waliosahaulika ili muziki huo urudi tena Kama ilivyokuwa zamani.

"Tukiwapa njia nzuri na kuwarudisha katika gemu wanamuziki hao na wao watainuka na kujiendeleza  kama ilivyo singeli kwa sasa imepiga hatua, vile vile pia hata makampuni mengine watahamasika  kuandaa matamasha makubwa  kwa wasanii hao" amesema Yakub.

Mratibu huyo amesema kwa sasa wataanzia katika Jiji la Dar es salaam huku wakiendelea kujipanga kujiandaa kwenda mikoa mingine zaidi na kufika nchini kote Tanzania.

Wasanii watakao toa burudani siku hiyo ni Dogo Niga,Jack Simela,Mczo,Jagwa dege la jeshi,Mzee wa bwax,Mfalme ninja,Yuda Msaliti,Ezy man,Segere,Majid Migomba na wasanii hao watasindikizwa na wasanii wangine ambao ni Sholo Mwamba,Manfongo,Dula Makabila pamoja na Mataluma mama mubaya.

Tamasha hilo la aina yake linatarajia kufanyika  Septemba 16 mwaka huu katika viwanja vya Leadars Jijini Dar es Salaam kuanzia  saa 3 asubuhi mpaka 12 jioni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...