Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba akifungua mkutano wa wadau wa Mazingira  Jijini Arusha. Mkutano huo umeshirikisha wadau mbalimbali kutoka Taasisi za Serikali na zile zisizo za kiserikali kwa lengo la kujadili changamoto ya mimea vamizi yenye athari hapa nchini.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba akifuatilia mawasilisho ya mimea vamizi kutoka kwa Mtaalamu wa COSTECH (hayupo pichani). Kulia ni Mhe. Nape Nnauye Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi na Maliasili.
Sehemu ya Washiriki wa Mkutano wa wadau wa kujadili changamoto za mimea vamizi. Mkutano umefanyika katika ukumbi wa AICC jijini Arusha. Mstari wa mbele katika picha ni waheshimiwa wabunge waliohudhuria.


KATIKA jitahada za kupambana na mimea vamizi nchini ambayo kwa kiasi kikubwa ina athari kwa uchumi wa Nchi yetu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba hii leo amewakutanisha wadau kutoka sekta mbalimbali, asasi za kiserikali na zisizo za kiserikali, Wenyeviti wa Kamati za Bunge za Ardhi na Maliasili, Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji ili kwa pamoja waweza kujadili namna bora ya kupambana na mimea vamizi ambayo imetapakaa kwa kasi katika maeneo mbalimbali hapa nchi.

“Pamoja na kwamba viumbe vamizi wageni ni janga kwa makazi asilia ya viumbe, lakini hatujalishughulikia kikamilifu, kuweka mikakati madhubuti ya kuzuia na kukabiliana na viumbe hivi. Kwa muktadha huo, leo tumepata fursa adimu na adhimu kutafakari kuhusu hali ilivyo kwa sasa, changamoto zilizopo na kujadili mikakati madhubuti ya kukabiliana na tatizo la viumbe vamizi wageni hapa nchini” Makamba alisisitiza.

Wadau waliohudhuria mkutano huo wameitaka Serikali kuongeza nguvu katika kupambana na tatizo hilo kwa kuibua miradi mbalimbali kote nchini ili kwa pamoja kuwa na mkakati wa kitaifa wa kupambana na hali hiyo ambayo ina athari kubwa kiutalii.

Mhe. Innocent Bashungwa Makamu mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira amesema kuwa suala kubwa ni kuuongeza bajeti kila mwaka katika sekta ya usimamizi wa mazingira pamoja na kuanzishwa kwa Mfuko wa Mazingira.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...