Serikali imetaka  wazazi,walimu wakuu,watendaji wa kata na vijiji pamoja wale wote watakaousika na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto au kumpa mimba mwanafunzi kuwajibiswa kwa kusababisha watoto wa kike kushindwa kumaliza masomo yao na kusababisha wasichana walio mashuleni kushindwa kutimiza ndoto zao.                                                                                                           
Hayo yalisemwa jana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile alipofanya ziara Mkoani Morogoro kupata taarifa ya Mkoa huo kwa lengo la kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa masuala Afya na Maendeleo ya Jamii Mkoani humo.

Akizungumzia hali hiyo Naibu Waziri Ndugulile alisema kiwango cha matukio haya ni kikubwa mno na kuagiza Mkoa huo kuanzisha Madawati ya Ulinzi na Usalama ya Wanawake na Watoto pamoja na vituo vya mkono kwa mkono (One Stop Centres) akisistiza kuwa haya ni maagizo ya serikali kama sehemu muhimu ya kupambana na vitendo vya ukatili nchini. 

“Vituo hivi kwa nchi nzima ni kumi kwa hiyo akikisheni mnaanzisha Vituo hivi katika Mkoa wa Morogoro kwa kuwa ili ni agizo la serikali katika kuakikisha tunatokomeza vitendo vya ukatili”. Aliongeza Dkt.Ndugulile.

Akisoma taarifa ya Mkoa huo kwa Naibu Waziri Ndugulile, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Frank Jacob alisema kuwa mkoa wa Morogoro una jumla ya matukio 2,555 ya mimba za utotoni akiyataja matukio 1,160 kuripotiwa kutoka Dawati la Polisi mengineyo 895 kulipotiwa katika vituo vya Afya, mashuleni na jamii.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na viongozi wa mkoa wa Morogoro na baadhi ya watumishi wa Mkoa huo hawako pichani kuhusu madhumni ya kuanza ziara ya siku tatu mkoani humo pia kupokea taarifa ya masuala ya Afya na Maendeleo ya Jamii ya Mkoa jana huo.
2
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akitoa ufafanuzi wa hali ya maendeleo sekta Afya na Maendeleo ya Jamii ya Mkoa wa Morogoro kwa  Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile kabla ya Waziri huyo kuanza ziara ya siku tatu Mkoani humo .
3
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Frank Jackob akitoa taarifa ya Mkoa wa Morogoro kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipotombelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kupata taarifa ya Mkoa huo kabla ya kuanza ziara yake ya siku tatu  Mkoani humo.
4
Baadhi ya watumishi wa Mkoa wa Morogoro wakifuatilia kwa makini maelezo na maagizo ya Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipotembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo kabla ya kuanza ziara ya siku tatu Mkoani humo.
Picha Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...