- Wateja kupata fursa kutoa mawazo kuboresha huduma.


Ikiwa katika shamrashamra ya kuadhimisha miaka 3 ya utoaji wa huduma kwa watanzania, Kampuni ya mawasiliano ya simu ya Halotel, kwa mara ya kwanza imetangaza mpango wa kutoa huduma ya zawadi kwa wateja wake ambao watatoa mawazo katika kusaidia uboreshaji wa huduma kwa wateja.

Mpango huo uliopewa jina la “LONGA TUSONGE” pamoja na faida zingine una lengo la kuwashirikisha wateja wote pamoja na wafanyakazi wa Halotel katika kufanya maboresho ya utoaji huduma mbalimbali kupitia mawazo yao wakati huu ambapo kampuni hiyo inapoadhimisha miaka mitatu ya utoaji huduma zake za Mawasiliano hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa mpango huo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Kampuni hiyo, Mhina Semwenda, amesema kuwa, mkakati huo ni sehemu ya kuthamini mchango mkubwa wanaoutoa wateja wake tangu kuanza kutolewa kwa huduma kupitia mtandao huo hapa nchini .

Amesema tangu kuingia kwa huduma za Mtandao huo wa Halotel, wamekuwa wakipata matokeo mazuri ya wateja wake wanaondeelea kutumia huduma zake mbalimbali hadi wakati huu ambapo wanakuja na mpango huo mpya wa “LONGA TUISONGE”

Amesema kupitia mpango huo wa mwaka mmoja, wateja wa mtandao huo watapewa nafasi ya kutoa mawazo yao mbalimbali ya kuboresha huduma za Halotel ambayo baadae yatachujwa na kwa yale yatakayokidhi matakwa yatapitishwa na kuwa huduma rasmi ndani ya mtandao huo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Halotel Mhina Semwenda,(kushoto) akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa mpango wa kutoa ya zawadi kwa wateja wake ambao watatoa mawazo katika kusaidia uboreshaji wa huduma kwa wateja uliopewa jina la Longa Tusonge. Kulia ni Msaidizi wa Mkuu wa kitengo cha Huduma kwa wateja Anthony Thobias.
Msaidizi wa kitengo cha Huduma kwa wateja Anthony Thobias ( kushoto) akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa mpango wa kutoa ya zawadi kwa wateja wake ambao watatoa mawazo katika kusaidia uboreshaji wa huduma kwa wateja uliopewa jina la “Longa Tusonge”. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Halotel Mhina Semwenda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...