????????????????????????????????????
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa (kulia), akikabidhi hundi kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Prof. Lucian Msambichaka baada ya kununua hisa za benki hiyo muda mfupi baada ya DCB kuzindua zoezi la uuzaji wa hisa kwa mwaka 2018, jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.Uzinduzi huu unawalenga wanahisa waliopo, wawekezaji wapya na umma wa watanzania ikizingatiwa kuwa kwa mara ya mwisho DCB ilitoa fursa kama hiyo mwaka 2012.
UONGOZI wa Benki ya DCB umetangaza rasmi kuanzia Novemba 12 mwaka huu kuanza hisa zake kwa wanahisa wa sasa na umma wa Watanzania kwa ujumla na kwamba uuzaji wa hisa hizo umegawanyika kwenye awamu mbili.
Wakizungumza wakati wanatangaza uuzaji wa hisa hizo jijini Dar es Salaaam uongozi wa benki hiyo umesema hiyo ni fursa ya kipekee ambayo wanahisa na watanzania wote wanatakiwa kuichangamkia na kwamba hisa moja itauzwa kwa bei ya Sh.265 ambayo ni cheni ya bei iliyopo kwenye Soko la Hisa Dar es Salaam(DSE).
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Biashara ya DCB Godfrey Ngalahwa amesema kuwa "Nachukua nafasi hii kuwataarifu kuwa uuzaji wa hisa za DCB unatarajia kuanza leo 12 Novemba 12, 2018. na kwamba Novemba 5, 2018, Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) ilitoa idhini ya uuzaji wa hisa kwa wanahisa wa sasa na umma wa Watanzania kwa ujumla.
"Dhana kubwa ni kuwaruhusu wanahisa waliopo kununua hisa na kutoa nafasi kwa wawekezaji wengine kununua hisa zitakazobaki. 
Kwa habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...