CBA Bank na Vodacom wamefanya promosheni ya pili ya Mpawa iliyoibua washidi wengine 200 walioweka amana na Mpawa , Ambao watajishindia mara mbili ya kiasi walichohifadhi kwenye Mpawa. 

Promotion hii ilizinduliwa tarehe 8 mwezi wa kumi na moja, Draw ya leo inafanya idadi ya washindi kuwa 430, Ambapo washindi 400 wamejishindia mara mbili ya amana zao walizohifadhi kwenye Mpesa, na washindi 30 ambao walikopa na kurejesha kabla ya wakati wamejishindi Shilingi TZS 100,000/= kila mmoja. 
 
Jumla ya washidi 1296 wanategemea kupatikana katika kipindi hiki cha wiki sita za kampeni. Zawadi kubwa zitakazotolewa kwenye droo kubwa wiki ya sita zitakua ni kitita cha Milioni 10 taslimu na Bajaj tano.

Promosheni hii inaonyesha jitihada za CBA Bank na Vodacom kuleta muamko wa kifedha na kuhimiza Watanzania kuwa na tabia ya kuweka akiba. Akizungumza wakati wa uzinduzi kutoa zawadi kwa washindi wa droo ya kwanza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa CBA Julius Konyani alisema “M-PAWA ni bidhaa inayoendelea kuleta mapinduzi ya kimaendeleo kwa Watanzania hasa wale wamiliki wa biashara ndogo wanaoweka akiba na na kupata riba na Pia kupata mikopo inayowasaidia katika kuendeleza na kukuza biashara zao”.

Promosheni hii ya Shinda na M-PAWA itaendeshwa kwa muda wa wiki sita kuanzia Novemba 2018 hadi nusu ya Desemba 2018. Meneja Masoko wa Vodacom Huduma za kifedha Noel Mazoya alisema “Wateja watakaoomba mkopo na kurudisha mapema watakuwa na nafasi ya kuopoa zawadi ya shilingi 100,000 kwa wateja 15 kila wiki na Jumla ya wateja 96 watashinda kwa wiki sita. 
 
Mkurugenzi Idara Wateja binafsi na Masoko wa Benki ya Biashara Afrika CBA Julius Konyani(katikati), na muwakilishi kutoka Vodacom Tanzania Noel Mazoya, katika katika uzinduzi rasmi wa Promosheni iliyopewa jina la Shinda na M-PAWA. ilifatwa na kutangazwa kwa washindi 400 waliongezewa mara mbili ya salio lao, na watu 30 zaidi waliochukua mikopo na kulipa kwa wakati walijishindia 100,000 tshs kila mmoja.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...