Na Mwandishi wetu
MKUU wa wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo amewataka wasichana kutumia fursa za uwapo wa Tehama kutimiza ndoto zao.
Ushauri huo aliutoa mwishoni mwa wiki wakati alipozungumza na wasichana wa sekondari waliokuwa katika jukwaa la ujasiriamali kwa wasichana.
Jumla ya wasichana 156 kutoka shule 25 za Dar es salaam walijumuika kwa siku mbili katika jukwaa ambapo miradi yao iliyobuniwa kwa kutumia teknolojia ilifanyiwa uhakiki na mshindi kupewa tuzo.
Katika jukwaa hilo lililoendeshwa na shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama Apps and Girls likishirikiana na Ubalozi wa Marekani hapa nchini, Jokate Mwegelo alisema wasichana wa nguvu kubwa ya kuleta mabadiliko katika maisha yao na jamii zao wanachotakiwa ni kutumia fursa zilizopo vizuri.
Alisema mafunzo ambayo wasichana hao wameyachukua ni fursa nzuri ya kujibadilisha na kusema hawana sababu ya kuwa waoga katika hilo bali wajitume inavyostahili.
Alisema katika utekelezaji wa ndoto zao kunakuwa na vikwazo vingi lakini ni wajibu wao kuvishinda na kusonga mbele.
Alitolea mfano yeye ambapo baada ya kusoma alisimama kidogo na kuwaambia wazazi wake kwamba anasimama kidogo ili atengeneze bidhaa ambazo zingeweza kumfanya kutimiza ndoto yake.
Alisema japokuwa wazazi wake hawakumwelewa alikazania alichofikiri na ndio chanzo cha kidoti, alama inayotambuliwa na watu wengi.
Alisema baada ya mafunzo yao ni vyema wakatambua na kujitambua wao wanaweza nini ili waweze kuwa juu.
“Haiwezi kuwa rahisi hata Yesu alibeba msalaba wake kukomboa watu wake” alisema akimaananisha kwamba ni vyema kuwa na maono ya unachotaka kama unataka kushiriki vyema.
Alisema kwamba wamejifunza elimu ya dijiti kama vile programu za Kompyuta (coding) na ujasiriamali wanachotakiwa kukifanya ni kufanya ubunifu wa miradi inayohusisha teknolojia na kuitumia mitandao ya kijamii kwa manufaa yao kwa kuwa mitandao inaunganisha dunia.
Alisema kwamba kama mtoto wa kike akijielewa atatumia vyema fursa za uwekezaji zilizopo kwa kutumia vyema elimu anayoipta na kujiingiza katika ujasiriamali.
MKUU wa wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo amewataka wasichana kutumia fursa za uwapo wa Tehama kutimiza ndoto zao.
Ushauri huo aliutoa mwishoni mwa wiki wakati alipozungumza na wasichana wa sekondari waliokuwa katika jukwaa la ujasiriamali kwa wasichana.
Jumla ya wasichana 156 kutoka shule 25 za Dar es salaam walijumuika kwa siku mbili katika jukwaa ambapo miradi yao iliyobuniwa kwa kutumia teknolojia ilifanyiwa uhakiki na mshindi kupewa tuzo.
Katika jukwaa hilo lililoendeshwa na shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama Apps and Girls likishirikiana na Ubalozi wa Marekani hapa nchini, Jokate Mwegelo alisema wasichana wa nguvu kubwa ya kuleta mabadiliko katika maisha yao na jamii zao wanachotakiwa ni kutumia fursa zilizopo vizuri.
Alisema mafunzo ambayo wasichana hao wameyachukua ni fursa nzuri ya kujibadilisha na kusema hawana sababu ya kuwa waoga katika hilo bali wajitume inavyostahili.
Alisema katika utekelezaji wa ndoto zao kunakuwa na vikwazo vingi lakini ni wajibu wao kuvishinda na kusonga mbele.
Alitolea mfano yeye ambapo baada ya kusoma alisimama kidogo na kuwaambia wazazi wake kwamba anasimama kidogo ili atengeneze bidhaa ambazo zingeweza kumfanya kutimiza ndoto yake.
Alisema japokuwa wazazi wake hawakumwelewa alikazania alichofikiri na ndio chanzo cha kidoti, alama inayotambuliwa na watu wengi.
Alisema baada ya mafunzo yao ni vyema wakatambua na kujitambua wao wanaweza nini ili waweze kuwa juu.
“Haiwezi kuwa rahisi hata Yesu alibeba msalaba wake kukomboa watu wake” alisema akimaananisha kwamba ni vyema kuwa na maono ya unachotaka kama unataka kushiriki vyema.
Alisema kwamba wamejifunza elimu ya dijiti kama vile programu za Kompyuta (coding) na ujasiriamali wanachotakiwa kukifanya ni kufanya ubunifu wa miradi inayohusisha teknolojia na kuitumia mitandao ya kijamii kwa manufaa yao kwa kuwa mitandao inaunganisha dunia.
Alisema kwamba kama mtoto wa kike akijielewa atatumia vyema fursa za uwekezaji zilizopo kwa kutumia vyema elimu anayoipta na kujiingiza katika ujasiriamali.
Mkuu
wa Wilaya ya Kisarawe, Mh. Jokate Mwegelo akizungumza kutia hamasa
wasichana wa shule mbalimbali za sekondari nchini wakati wa jukwaa la
kufunza wasichana wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES
2018) lililoandaliwa Shirika lisilo la kiserikali la ‘Apps and Girls’
kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani lililomalizika jana katika
ukumbi wa American Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa.
Mtaalamu
wa Mawasiliano katika Sekta ya Nishati kutoka Kampuni ya Uendelezaji
Jotoardhi Tanazania, Johary Kachwamba akiwasilisha fursa za ubunifu
katika sekta ya nishati wakati wa jukwaa la kufunza wasichana
wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa
shirika lisilo la kiserikali la ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na
Ubalozi wa Marekani lililomalizika jana katika ukumbi wa American Corner
uliopo Maktaba Kuu ya Taifa.
Afisa
Mipango wa Reach for Change Foundation, Bi. Jesca Mmari akizungumza na
wanafunzi akiwataka kuwa na hamu na kujiamini katika kila kitu
wanachotaka kukipata wakati wa jukwaa la kufunza wasichana wajasiriamali
(Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa shirika lisilo
la kiserikali la ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na Ubalozi wa
Marekani lililomalizika jana katika ukumbi wa American Corner uliopo
Maktaba Kuu ya Taifa.
Mtalaamu
wa Jinsia na Vijana kutoka Shirika la Misaada la Marekani nchini
(USAID), Bi. Shamsa Suleiman akizungumzia kazi mbalimbali zinazofanywa
na shirika lake wakati wa jukwaa la kufunza wasichana wajasiriamali
(Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa shirika lisilo
la kiserikali la ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na Ubalozi wa
Marekani lililomalizika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa American
Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Afisa
Rasilimali watu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. John Mtega
(kushoto) akizungumzia usawa wa kijinsia katika ajira na kuhamasisha
wanawake kuomba nafasi za utumishi wakati wa jukwaa la kufunza wasichana
wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa
na shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama ‘Apps and Girls’ kwa
kushirikiana na Ubalozi wa Marekani lililomalizika mwishoni mwa wiki
katika ukumbi wa American Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa jijini Dar
es Salaam. Wengine katika picha ni Mhandisi wa Umeme kutoka Shirika la
Umeme Tanzania (TANESCO), Bi. Mkufu Shabaan (wa pili kushoto), Mtalaamu
wa Jinsia na Vijana kutoka Shirika la Misaada la Marekani nchini
(USAID), Bi. Shamsa Suleiman (wa pili kulia) pamoja na Afisa Mipango wa
Reach for Change Foundation, Bi. Jesca Mmari (kulia).
Washindi
wa kwanza wa shindano la ubunifu wa programu za kompyuta, ambao
waliwasilisha wazo la changamoto za ukosefu wa taulo za watoto kike
mashuleni wakiwa katika picha ya pamoja na Afisa anayeshughulikia
Utamaduni kutoka Ubalozi wa Marekani, Bw. Jeffrey Ladenson (wa tatu
kushoto), Mwanzilishi mwenza wa Apps & Girls, Bi. Carolyne
Ekyarisiima (kushoto) na majaji wa shindano hilo wakiongozwa na Jaji
Kiongozi wa shindano hilo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Lyra in Africa,
Bi. Roselyne Mariki (wa tatu kulia) wakati wa jukwaa la kufunza
wasichana wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018)
lililoandaliwa shirika lisilo la kiserikali la ‘Apps and Girls’ kwa
kushirikiana na Ubalozi wa Marekani na kufanyika mwishoni mwa juma
katika ukumbi wa American Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa jijini Dar
es Salaam. Washindi hao ni Eshe Mohamed (wa pili kushoto), Oliver
Godliving (wa nne kushoto), Maleo Stanley (wa tano kulia) pamoja na
Mwalimu Msimazi, Celestina Richard (wa nne kulia) kutoka shule ya
Sekondari Kondo iliyopo jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...