NA TIGANYA VINCENT,RS TABORA 

JUMLA ya Madaktari Bingwa 42 wanatarajia kutoa huduma ya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali ikiwemo tezi dume na kansa ya matiti kwa wakazi wa Wilaya ya Urambo kuanzia wiki ijayo. 

Kauli hiyo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Urambo Magreth Sitta wakati akitoa taarifa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani jan. Alisema madaktari hao watato huduma ya uchunguzi wa dezi dume kwa wanaume na uchunguzi wa satani ya matiti kwa wanawake kutoka maeneo mbalimbali wilayani humo. 

“Nawaombeni Waheshimiwa Madiwani fikisheni ujumbe huu kwa watu wenu ili wakazi wengi kujitokeza kupata huduma hizo…haitakuwa vizuri Madaktari bingwa wamekuja kutoa huduma kwetu kasha wakute hakuna watu.”alisema. Alisema zoezi limeandaliwa na Ofisi ya Mbunge kwa kushirikiana na Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kwa lengo la kuhakikisha wakazi wake wanapata huduma ya uchunguzi huduma karibu yao. 

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Urambo alisema kuwa huduma zitakazotolewa ni pamoja uchunguzi wa tezi dume, uchunguzi wa saratani ya matiti kwa wakinamama na macho. Alisema wameamua kutoa huduma hizo pamoja na uchunguzi wa tezi dume ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya Marehemu Spika Mstaafu Samwel Sitta kwa kuwa tatizo hilo ndilo lilisababisha kupoteza maisha. 

Mganga huyo wa Wilaya aliwataka wananchi wengi kujitekeza kupata huduma hizo Urambo kwani nje ya hapo katika Hospitali nyingine kama ile ya Taifa Muhimbili, Bugango na KCMC ni kubwa.
Mbunge wa Jimbo la Urambo Magreth Sitta akichangia taarifa ya utekelezaji wa kila Kata wilayani Urambo wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Urambo jana. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...