Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imepokea msaada wa vifaa tiba aina ya Stents vyenye thamani ya Tshs. 86.2 milioni kutoka kampuni ya Boston Scientific ya Marekani kwa ajili ya wagonjwa wenye tatizo la saratani ya koo la chakula. 

Stents ni vifaa maalum mithili ya springi ambavyo vinaweza kuwa vya plastiki au chuma vyenye uwazi katikati wanavyowekewa wagonjwa wenye uvimbe kwenye koo lililoziba ili kupanua sehemu hiyo na kuruhusu kupitisha chakula. Kuna stents za aina mbalimbali kutegemeana na mgonjwa ana shida ya aina gani. 

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Magonjwa ya Mfumo wa Chakula na Ini, Dkt. Masolwa Ng’wanasayi amesema kampuni hiyo imetoa stents 25 ambazo zitatumika kwa wagonjwa 25 wenye satarani ya koo la chakula ili kuwasaidia kumeza chakula na kuendelea na matibabu ya mionzi. 

“Mgonjwa mwenye tatizo la saratani ya koo la chakula, anakuwa hawezi kumeza chakula na hali hii inasababisha mgonjwa kupungua uzito na kushindwa kuendelea na matibabu mengine, hivyo vifaa hivi vitawasaidia kumeza chakula na kuendelea na matibabu mengine,” amesema Dkt. Ng’wanasayi. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Hopitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Lawrence Museru akipokea kifaa tiba cha aina ya STENTS kwa ajili ya wagonjwa wenye tatizo la saratani ya koo la chakula kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Boston Scientific ya Marekani, Troy Lengel. Wengine kushoto ni wawakilishi kutoka hospitali ya Muhimbili, Mayo Clinic ya Marekani na Chuo Kikuu cha San Francisco nchini Marekani na kulia ni wawakilishi kutoka MUHAS na Hospitali ya Muhimbili.
Pichani ni vifaa tiba aina ya STENTS ambavyo wagonjwa wenye tatizo la saratani ya koo la chakula wameanza kuwekewa ili kuwasaidia kumeza chakula kutokana na mfumo wa koo kuharibiwa na ugonjwa huo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...